Facebook

Tuesday, 23 December 2014

Mfanyabiashara maarufu kutoka Kenya anayejihusisha na ujangili akamatwa Tanzania.

 
Polisi wa kimataifa , interpol tawi la Tanzania wamemkamata mfanya biashara maarufu raia wa Kenya kwa tuhuma za kujihusisha na ujangili na uhalifu uliovuka mipaka ,hususan mauaji ya tembo .
mtuhumiwa huyo Mohamed Ally Feisal Amekamatwa mjini Dar-Es-Salaam baada ya kusakwa kwa kipindi kirefu kwa makosa hayo ya kimataifa kutoka Dar Regina Mziwanda anaarifu zaidi.
Akitbibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo Bwana Diwani Athumani kutoka kamisheni ya Kurugenzi ya makos aya jinai amesema mtuhumiwa huyo anakabiliwa na tuhuma za kujihusisha na vitendo vya uhalifu wa kimataifa ikiwemo uwindaji wa uliovuka mipaka kimataifa katika nchi mbali mbali)

Bwana Athumani Diwani alieleza kuwa kwa sasa mtuhumiwa huyo anashikiliwa huku upelelezi ukiendelea kujua makosa mengine aliyoyafanya kuhusiana na biashara za bidhaa zitokanazo na Tembo ndani ya Tanzania na katika nchi nyingine za Afrika Mashariki ikiwemo nchi yake ya asili Kenya.
Mohamed Feisal Ally amekuwa akitafutwa kwa muda mrefu kwa tuhuma za uwindaji haramu husani mauaji ya Tembo tatizo ambalo ni kubwa hususani katika ukanda huu wa Afrika Mashariki hasa Kenya na Tanzania ambapo idadi kubwa ya Tembo wamekuwa wakiuawa kila mwaka na kutishia kutoweka kwa viumbe hao.

Related Posts:

  • Sudan kusini yakabiliwa na baa la njaa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea uhaba wa chakula nchini Sudan Kusini kama mbaya zaidi kuwahi kuonekana duniani na kuyataka mataifa ambayo yaliahidi kutoa msaada wa zaidi ya dola millioni mia sita ku… Read More
  • Mama anayeugua Ebola atoroshwa Mwanamke aliyeambukizwa Ebola atoroshwa Hospitalini huko Freetown Hali ya Tahadhari imetangazwa mjini Freetown Sierra Leone baada ya mwanamke mmoja aliyeambukizwa Ebola kutoroshwa kutoka Hospitalini na jamaa zake kw… Read More
  • Juhudi za kutafuta amani Gaza zaingia dosari. Wapalestina zaidi ya 800 wameuawa na Waisraeli 35 Israeli imeendelea kuivirumishia makombora Gaza kucha kutwa ,huku kikao cha mawaziri wa baraza la Usalama kikitarajiwa huko Marekani kujadili mapendekezo mapya ya … Read More
  • Sudan kusini yakabiliwa na baa la njaa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea uhaba wa chakula nchini Sudan Kusini kama mbaya zaidi kuwahi kuonekana duniani na kuyataka mataifa ambayo yaliahidi kutoa msaada wa zaidi ya dola millioni mia sita ku… Read More
  • Maandamano yazuka Palestina polisi wakabiliana na raia Palestina Maandamano makubwa yamefanyika katika ukingo wa Magharibi mwa Palestina karibu na mpaka wake na Israel kupinga mashambulio yanayofanywa na Israel. Waandamanaji hao wakiwa na hasi… Read More

0 comments:

Post a Comment