Facebook

Monday 29 December 2014

Vigogo wa Ligi England waambulia sare

Vigogo Manchester City,Chelsea na Man United wamejikuta wakiambaulia sare katika michezo yao ya ligi ya England.
Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu Manchester City waliambulia sare baada ya kuruhusu timu ya Burnley kurudisha mabao mawili yaliyofungwa kipindi cha kwanza na mchezo kumalizika kwa sare ya 2-2.
Huku vinara wa ligi hiyo Chelsea wakipata sare ya bao 1-1 dhidi ya Southampton. Sadio Mane aliipa Southampton Bao la kuongoza kabla ya Eden Hazard kuisawazisha timu yake Sekunde chache kabla ya mapumziko.
Manchester United wakiwa ugenini kwenye uwanja wa White Hart Lane walishindwa kutamba mbele ya Tottenham kwa kukubali kutoka sare ya 0-0.

Matokeao ya michezo mingine
Aston Villa 0 - 0 Sunderland
Hull City 0 - 1 Leicester City
Queens Park Rangers 0 - 0 Crystal Palace
Stoke City 2 - 0 West Bromwich Albion
West Ham United 1 - 2 Arsenal
Newcastle United 3 - 2 Everton

Matokeo haya bado yanawabakisha Chelsea kileleni mwa Ligi mbele ya Timu ya Pili Mabingwa Watetezi Man City wakifuatiwa na Man United waliuoko nafasi ya tatu.

0 comments:

Post a Comment