Wednesday, 30 July 2014
Askofu: Chikawe huna ubavu wa kulifuta kanisa langu.
Askofu Kiongozi wa Kanisa la
Moravian nchini, Alinikisa Cheyo amesema
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe
hana ubavu wa kulifuta kanisa lake.
Cheyo alitoa kauli hiyo jana ikiwa ni siku
moja baada ya Waziri Chikawe kutishia
kulifuta kanisa hilo na madhehebu mengine
yatakayoendekeza migogoro.
Akizungumza Dar es Salaam kwenye
maombezi ya kuliombea Taifa yaliyoandaliwa
na Jumuiya ya Karismatiki Katoliki Jimbo Kuu
la Dar es Salaam juzi, Chikawe alisema Kanisa
la Moravian lina migogoro inayosababisha
hata waumini wake wapigane hadharani
wakati wa ibada.
“Ninawataka viongozi wa kanisa hili kumaliza
tofauti zao kupitia mabaraza yao ya ndani
badala ya kufikishana katika vituo vya polisi,
vinginevyo nitachukua hatua ya kulifuta kwa
kuwa yanahatarisha amani ya nchi,’’
alinukuliwa akisema Chikawe.
Kutokana na kauli hiyo, Askofu Kiongozi huyo
alijibu jana akisema: “Waziri hana uwezo wa
kufuta kanisa kwani ni la Mungu, lakini
migogoro itamalizwa na sisi wenyewe.”
Kwa kipindi kirefu kanisa hilo limekuwa na
migogoro maeneo ya Tabata na
Mwananyamala, Dar es Salaam na Jimbo la
Kusini Mbeya.
Hivi karibuni, wachungaji na waumini wa
kanisa hilo katika Jimbo la Mbeya walifunga
lango kuu la kuingia makao yake makuu na
kusababisha polisi na Mkuu wa Wilaya ya
Mbeya, Dk Norman Sigala kuingilia kati.
Kutokana na mgogoro huo, Kamati ya Ulinzi
na Usalama ya wilaya hiyo, ilifanya kikao cha
dharura na halmashauri ya kanisa hilo na
ilidokezwa kwamba walifikia mwafaka mzuri.
Hata hivyo, baada ya siku mbili kanisa hilo
liliwasimamisha kazi wachungaji watano
ambao nao kupitia kwa wakili walitoa siku
saba kwa makamu mwenyekiti aliyeandika
barua kuwarudisha kazini haraka.
Related Posts:
Usiombee Kuugua Dengue, Kipimo ni Sh50,000 Wakati taharuki iliyosababishwa na mlipuko wa homa ya dengue ikiendelea kutikisa kila kona ya jiji, imebainika kwamba gharama za vipimo katika hospitali mbalimbali zinafikia Sh50,000, ikiwa ni tofauti kubwa na Sh… Read More
Majina ya vijana wa mujibu wa sheria waliomaliza kidato cha sita 2014 waliochaguliwa kujiunga na JKT BUROMBOLA-KIGOMA VIJANA MUJIBU WA SHERIA KWENDA BUROMBOLA-KIGOMA S/NoMKOANAMBA YA SHULEJINA LA SHULEJINSIJINA 1 ARUSHA S0110 ILBORU SECONDARY SCHOOL M ABEL FRANCIS NGUGI 2 ARUSHA S0110 ILBORU SECONDARY SCHOOL M ABUBAKAR ALLY … Read More
Wito wa kupigwa marufuku waganga TZ Visa vya kuuawa kwa albino havijakoma Tanzania Polisi nchini Tanzania wamewakamata waganga wawili wa kienyeji baada ya mwanamke mmoja mwenye ulemavu w… Read More
TANGAZO:MAJINA YA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA (JKT) KWA MUJIBU WA SHERIA MWAKA - 2014 AWAMU YA KWANZA; VIJANA 20,000 WATARIPOTI KWENYE MAKAMBI YA MAFUNZO YA JKT KUANZIA TAREHE 01 JUNI 2014 NA KUANZA RASMI MAFUNZO YAO TAREHE 08 JUNI 2014 NA KUMALIZA TAREHE 04 SEPTEMBA 2014. ORODHA YAO… Read More
Njemba lanaswa na denti wa kiume gesti ISHARA za mwisho wa dunia? Njemba aliyetajwa kwa jina moja la Zeb amekula kichapo na kuishia mikononi mwa polisi baada ya kunaswa katika nyumba ya kulala wageni (gesti) akiwa na dogo wa kiume aliyedaiwa kuwa ni denti… Read More
0 comments:
Post a Comment