Facebook

Friday, 25 July 2014

Mwanariadha mwenye asili ya kiafrika aemjiondoa kutoshiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola



Mo Farah hatoshiriki mashindano ya jumuiya ya madola huko Glasgow
Mwanariadha raia wa Uingereza mwenye asili ya Somalia, Mo Farah amejiondoa kutoka mashindano ya Jumuiya ya Madola mjini Glasgow, Scotland.
Bingwa huyo mara mbili wa Olympiki amejiondoa katika mashindano hayo ya jumuiya ya madola kutokana na ushindwa kupona jeraha lake.
Hata hivyo ameamua kwendelea kuwepo katika kambi yake ya mazoezi kwa maandalizi ya mashindanoya kuwania ubingwa wa ulaya yatakayofanyika mwezi ujao mjini Zurich.
“nimechukua uamuzi huu mgumu wa kujiondoa katika mashindano haya ya commonwealth “amesema mwanariadha huyo wa kikosi cha Uingereza.
“Ningependelea kuongeza medali ya commonwealth kwenye medali zangu za ubingwa wa olympiki na ubingwa wa dunia ,lakini mashindano haya yamekuja mapema wakati bado naenndelea kuuguza jeraha na mwili wangu bado haujanikubalia kukimbia”

Mo Farah hatoshiriki mashindano ya jumuiya ya madola huko Glasgow
Wakati huo huo mashindano tayari yameanza,wachezaji wa Judo kutoka nchi za Kenya na Tanzania wapo uwanjani hii leo.
Pia wachezaji wa Table Tennis kutoka Uganda na Kenya wanatupa karata zao katika michuano ya mchujo inayofanyika katika viwanja mbali mbali jijini Glasgow.
Kwingineko, kuna ripoti kuwa wanariadha katika kambi ya kikosi cha Kenya wanasemekana kulalamikia hali duni ya kambi yao.
Baadhi yao wanasema kuwa hawana vifaa vya kimsingi na hali katika kambi hiyo ni mbaya.
Vile vile wamelalamika kuhusu kucheleweshwa kwa marupurupu yao lakini maafisa katika kambi hiyo ya Kenya wamesema masuala hayo ni ya ndani na wanayashughulikia.

Related Posts:

  • Berlusconi ashinda rufaa yake.   Waziri mkuu wa zamani wa Italy, Silvio Berlusconi, ameshinda rufaa yake dhidi ya mashtaka ya kulipa kufanya mapenzi na kahaba mwenye umri mdogo.    Majaji katika mahakama ya Milan wametupilia mbali… Read More
  • Afungiwa mechi 3 kwa kumpiga mwamuzi.   Mshambuliaji wa Zamalek Dominque da Sila amefungiwa na shirikisho la Soka la Afrika Caf kwa kumpiga mwamuzi. Tukio hilo lilitokea katika mechi ya Champions League kati ya Zamalek dhidi ya TP Mazembe tarehe 8 … Read More
  • REAL MADRID TIMU "TAJIRI" DUNIANI - FORBES Klabu ya kandanda ya Real Madrid ya Spain imeongoza katika orodha ya Forbes ya timu zenye thamani zaidi duniani. Real Madrid, walioshinda Champions League mwezi Mei, ina thamani ya takriban dola BILIONI 3.44, kwa mujibu … Read More
  • Nahodha wa Ujerumani astaafu kucheza soka la kimataifa.   Nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani Philipp Lahm amestaafu kucheza soka la kimataifa, baada ya kukiongoza kikosi chake na kushinda Kombe la Dunia nchini Brazil. Beki huyo wa Bayern Munich, ambaye pia anawez… Read More
  • UEFA yatangaza wachezaji watakaowania "Mchezaji bora wa Ulaya" UEFA Jana ilitoa Majina 10 ya Wagombea Tuzo yao ya Mchezaji Bora wa Mwaka na Mshindi atatangazwa hapo Agosti 28 wakati wa Droo ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI. Awali Majina ya Wachezaji 35 yalipigiwa Kura na hao 10 n… Read More

0 comments:

Post a Comment