Facebook

Monday 28 July 2014

Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya.

Salim Kikeke's photo.
West Ham wanataka kumsajili mshambuliaji wa Cameroon, Samuel Eto'o, 33 ambaye aliondoka Chelsea msimu uliopita (Sun on Sunday),
 Salim Kikeke's photo.
 Inter Milan wanafikiria kumtoa Fredy Guarin, 28, kubadilishana na Javier Hernandez, 26, kutoka Manchester United (Sun on Sunday), 
 Salim Kikeke's photo.
Romelu Lukaku aliyecheza Everton kwa mkopo msimu uliopita, anataka uhamisho wa kudumu kwenda Goodison Park (Talksport), 
 Salim Kikeke's photo.
Arsenal wanakaribia kukamilisha uhamisho wa kiungo wa Shakhtar Donetsk, Douglas Costa, 23 ambaye ameomba kuondoka Ukraine kwa sababu za matatizo ya kisiasa nchini humo (Caughtoffside),
 
Atlètico Madrid wamefikia makubaliano ya kumsajili Antoine Griezmann, 23 kutoka Real Sociedad kwa pauni milioni 24 (AS),
 
Meneja wa. Manchester United bado ana nia ya kumsajili kiungo wa Roma Kevin Strootman, 24, licha ya mchezaji huyo kuwa majeruhi kutokana na kuumia goti (Sky Sports),
 
Real Madrid wanapanga kumchukua Radamel Falcao, 28, kwa mkopo na uhamisho wa kudumu mwaka 2015 (AS), 
 
Jaribio la Stoke City kumsajili Oussama Assaidi, 25, kutoka Liverpool kwa pauni milioni 7, huenda likashindikana kutokana na winga huyo kutaka mshahara mkubwa (Daily Express), 
 
Mshambuliaji wa Lille Divock Origi, 19, anakaribia kukamilisha uhamisho wa pauni milioni 12.5 kwenda Liverpool (Sunday Mirror),
 
Sami Khedira anataka mshahara wa pauni milioni 7.1 kwa mwaka ili kujiunga na Arsenal (La Sexta),
 
Arsenal wanafikiria kupanda dau kumchukua kiungo wa Southampton Morgan Schneiderlin (Daily Star),
 
 Angel Di Maria anajiandaa kusaini mkataba wa miaka mitano siku chache zijazo na Paris St-Germain (Marca).

0 comments:

Post a Comment