Wednesday, 30 July 2014
SINEMA ZA UHAMIAJI ZAENDELEA - Kusitishwa kwa Ajira za Konstebo na Koplo
Baadhi ya Vyombo vya Habari leo tarehe 29
Julai, 2014 vimeandika kwa makosa kuwa ajira
za Uhamiaji zilizositishwa jana zinahusiana na
70 zilizopatikana baada ya usaili uliofanyika
katika Uwanja wa Taifa.
Ukweli ni kuwa usaili wa nafasi ya Mkaguzi
Msaidizi wa Uhamiaji ambao awali ulianzia
Uwanja wa Taifa ulienda vizuri hadi
wakapatikana wasailiwa wa kujaza nafasi 70 za
Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji. Zoezi hilo
halikuwa na matatizo yoyote, na waliochaguliwa
walitakiwa kuripoti kazini tarehe 29 Julai lakini
kwa sababu ya Sikukuu sasa wataripoti baada
ya sikukuu.
Hivyo tunapenda kufafanua kuwa wasailiwa
waliochaguliwa kujaza nafasi 70 za Mkaguzi
Msaidizi wa Uhamiaji hawahusiki na usitishwaji
uliotangazwa jana na wanatakiwa kuendelea na
mipango ya kuripoti kazini kama ilivyotangazwa
hapo awali.
Wasailiwa wanaohusika na kusitishwa kwa ajira
zao ni wale waliokuwa wameshiriki katika zoezi
la kuajiri Konstebo na Koplo wa Uhamiaji ambao
idadi yao ni 200, ambao walitakiwa kuripoti
tarehe 06 Agosti, 2014 lakini kwa sasa hawa
ndio wanaelekezwa wasubiri hadi hapo
watakapopewa maelekezo mengine.
Sgn
Isaac J. Nantanga
MSEMAJI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI
YA NCHI
29 JULAI, 2014
Related Posts:
Majambazi yavamia Kizuizi cha Polisi na sheli huko Kongowe-Mkuranga hivi punde.Habari zilizotufikia BantuTz.com hivi punde kutoka eneo la Kongowe-Mkuranga mkoani Pwani. Ni kwamba Majambazi wamevamia kizuizi cha polisi katika eneo la kongowe na kuuwa askari polisi wawili na kupora bunduki aina ya SMG mbi… Read More
BAADA YA ZITTO KABWE,AFANDE SELE NAE AJIUNGA RASMI ACT TANZANIA.Baada ya hapo jana aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA Zitto Zubery Kabwe kuhamia chama cha ACT TANZANIA. Leo hii aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA, msanii maarufu na Mfalme wa Rhymes Tanzania Afande Sele amehama rasmi CHADEMA na k… Read More
SAKATA LA ESCROW LAMBURUZA KIGOGO WA RITA MAHAKAMANI. Afisa Mtendaji MKuu wa Mamlaka ya Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) Phillip Saliboko amefikishwa mahakamani kwa kupokea fedha kiasi cha shilingi milioni 40, zilizochotwa kutoka akaunti ya Tegeta Escrow. … Read More
BAADA YA ZITTO KABWE,AFANDE SELE AJIUNGA RASMI ACT TANZANIA.Baada ya hapo jana aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA Zitto Zubery Kabwe kuhamia chama cha ACT TANZANIA. Leo hii aliyekuwa mwanachama wa CHADEMA, msanii maarufu na Mfalme wa Rhymes Tanzania Afande Sele amehama rasmi CHADEMA na k… Read More
Dereva wa bodaboda anusurika kuuawa baada ya kupora mkoba.kijana mmoja wa bodaboda maeneo ya Sinza Afrikasana jijini DSM ambaye jina halikupatikana, alikoswakoswa kuuawa baada ya kupora mkoba uliokuwa na simu ya mwanamke aliyekuwa akipita njia. Cha ajabu kijana huyo alivyokwapua mk… Read More
0 comments:
Post a Comment