Facebook

Thursday 24 July 2014

Shambulio katika kikosi cha Kumlinda Rais wa DRC lashundikana.

 Photo: SHAMBULIO KATIKA KIKOSI CHA RAIS DRC
Shambulio katika kambi ya jeshi ya kikosi cha kumlinda rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo limezuiwa, kwa mujibu wa maafisa wa serikali.
Hali imerejea kuwa ya utulivu na kundi dogo la "waliojipenyeza" limezidiwa nguvu, imesema serikali ya Kinshasa.
Milio mizito ya bunduki ilisikika katika kambi ya Tshatshi, kwa karibu dakika 30.
Mamlaka hazijasema nani amehusika na shambulio hilo.
Wakazi wa eneo hilo walihamishwa, na uwanja wa ndege wa kimataifa kufungwa.
Mlinzi mmoja wa kikosi cha rais ameliambia shirika la habari la AFP kuwa watu 20 waliokuwa na mavazi ya kiraia wamezidiwa nguvu.
Mwanajeshi mwingine ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa washambuliaji wanne wameuawa.
Shambulio katika kambi ya Tshatshi mwezi Disemba mwaka jana pia lilidhibitiwa.
Shambulio katika kambi ya jeshi ya kikosi cha kumlinda rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo limezuiwa, kwa mujibu wa maafisa wa serikali.
Hali imerejea kuwa ya utulivu na kundi dogo la "waliojipenyeza" limezidiwa nguvu, imesema serikali ya Kinshasa.
Milio mizito ya bunduki ilisikika katika kambi ya Tshatshi, kwa karibu dakika 30.
Mamlaka hazijasema nani amehusika na shambulio hilo.
Wakazi wa eneo hilo walihamishwa, na uwanja wa ndege wa kimataifa kufungwa.
Mlinzi mmoja wa kikosi cha rais ameliambia shirika la habari la AFP kuwa watu 20 waliokuwa na mavazi ya kiraia wamezidiwa nguvu.
Mwanajeshi mwingine ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa washambuliaji wanne wameuawa.
Shambulio katika kambi ya Tshatshi mwezi Disemba mwaka jana pia lilidhibitiwa.

0 comments:

Post a Comment