Facebook

Wednesday 23 July 2014

Rais wa Nigeria amekutana na wazazi wa wasichana waliotekwa nyara na Boko Haram.

Hatimaye Rais Goodluck akutana na wazazi


Baadhi ya wazazi ambao watoto wao walitekwa nyara
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amekutana na wazazi wa wasichana waliotekwa nyara na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram.
Zaidi ya watu walihudhuria mkutano huo ambapo hata serikali iliwapangia usafiri kutoka makwao.
Hii ni mara ya kwanza kwa Rais kukutana na wazazi hao tangu wasichana kutekwa nyara.
Rais Jonathan amekosolewa sana kuwekewa shinikizo aongeze kasi katika jitihada za kuokoa wasichana hao waliotekwa nyara siku miamoja zilizopita.
Wazazi hao walijiondoa katika mkutano uliokuwa umepangwa kufanyika kati yao na Rais Jonathan wiki jana wakisema kuwa wanahitaji mwazo kushauriana na familia zengine za wale ambao watoto wao walitekwa.
Rais Jonathan amesema kuwa wazazi hao walichochewa na wanaharakati ambao aliwatuhumu kwa kuingiza siasa katika swala hilo zima.
Baadhi wanamkosoa Rais Goodluck kwa kukosa kukutana na wazazi hao hadi aliposhinikizwa na Malala
Wakati hayo yakijiri watu 15,000 wametoroka makwao kutoka Kaskazini Mashariki mwa Nigeria mji wa Damboa baada ya ghasia zinazosababishwa na Boko Haram kukithiri.
Maafisa wanasema zaidi ya watu 40 wameuawa katika shambulizi lililofanywa na Boko Haram mjini humo Ijumaa.
Wapiganaji hao pia walishambulia vijiji vingine sita.
Kadhalika wapiganaji hao wamefanya mashambulizi mengine mjini Damboa ambako waliharibu milingoti na nyaya za stima na kuwaacha wakazi wa jimbo la Borno bila umeme kwa wiki kadhaa zilizopita.

"Mr Jonathan has been under pressure to meet the parents after being accused of handing the crisis badly.
Parents pulled out of a meeting with him last week amid accusations they were being used for political reasons.
The parents of 11 of the girls have died since their abduction by the Boko Haram group, the Associated Press news agency reports.
The abduction of the more than 200 schoolgirls sparked global outrage.
Brief prayer Boko Haram has offered to free the girls in exchange for the release of its fighters and relatives held by the security forces."

0 comments:

Post a Comment