Maelfu ya watu wametakiwa kutafuta hifadhi salama wakati tufani lenye nguvu likipita katika kisiwa cha Okinawa nchini Japan.
Tufani hilo lililopewa jina la Neoguri lilotarajiwa kukatisha katika kisiwa cha Okinawa siku ya Jumanne, likiandamana na upepo mkali na mvua kubwa.
Tufani hilo lililopewa jina la Neoguri lilotarajiwa kukatisha katika kisiwa cha Okinawa siku ya Jumanne, likiandamana na upepo mkali na mvua kubwa.

Watabiri wa hali ya hewa wanasema tufani hilo huenda likawa miongoni mwa kubwa zaidi kuwahi kuonekana Japan, likisababisha mawimbi yenye urefu wa hadi mita 14.
Mamlaka za huko zimewataka wakazi wake wapatao 480,000 kukaa ndani ya nyumba zao au kwenda katika vituo vya kijamii kutafuta hifadhi.

Tufani Neogori limeripotiwa kuonekana likielekea upande wa kaskazini kwa kasi ya kilomita 25 kwa saa likiwa na upepo unaovuma kwa kasi ya hadi kilomita 252 kwa saa, limeripoti shirika la habari la Kyodo.
0 comments:
Post a Comment