Facebook

Wednesday, 9 July 2014

Mamia wateketea na Ebola Afrika Magharibi.

 Photo: IDADI YA VIFO VYA EBOLA YAONGEZEKA
Maafisa wa afya wa Afrika Magharibi wanasema watu 25 zaidi wamekufa kutokana na maradhi ya Ebola tangu Julai 3, na kusababisha idadi ya waliokufa hadi sasa kufikia 518. Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema maambukizi mapya 50 yameripotiwa. Msemaji wa WHO amesema wafanyakazi wa huduma za afya wanapambana kujaribu kuudhibiti ugonjwa huo nchini Sierra Leone, Liberia na Guinea.
Siku ya Jumatatu, daktari mmoja nchini Ghana alisema vipimo vya awali kwa raia moja wa Marekani, havikuonesha kama ana ugonjwa huo.
Lakini vipimo zaidi vinaendelea kuchukuliwa.
Mtu huyo alikuwa ametembelea Sierra Leone na Guinea, na alikuwa amewekwa chini ya karantini baada ya kuonesha dalili za ugonjwa huo.

Maafisa wa afya wa Afrika Magharibi wanasema watu 25 zaidi wamekufa kutokana na maradhi ya Ebola tangu Julai 3, na kusababisha idadi ya waliokufa hadi sasa kufikia 518. Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema maambukizi mapya 50 yameripotiwa. Msemaji wa WHO amesema wafanyakazi wa huduma za afya wanapambana kujaribu kuudhibiti ugonjwa huo nchini Sierra Leone, Liberia na Guinea.
Siku ya Jumatatu, daktari mmoja nchini Ghana alisema vipimo vya awali kwa raia moja wa Marekani, havikuonesha kama ana ugonjwa huo.
Lakini vipimo zaidi vinaendelea kuchukuliwa.
Mtu huyo alikuwa ametembelea Sierra Leone na Guinea, na alikuwa amewekwa chini ya karantini baada ya kuonesha dalili za ugonjwa huo.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment