Facebook

Wednesday, 9 July 2014

Mfumo wa elektroniki kutumika mechi ya Taifa Stars na Msumbiji

Mechi ya kujipima nguvu kati ya Timu ya Taifa Stars na Msumbiji Julai 20 mwaka huu katika uwanja wa taifa, tiketi za kieletroniki kuanza kutumika na kiingilio katika mechi hiyo ni sh. 7000.
Afisa Habari wa Shirikisho la Kabumbu (TFF) Boniface Wambura alisema kuwa, tiketi hizo zitaaza kutumika ili kurahisisha usumbufu wa foleni kwa wapenzi wa mpira, kupewa fedha bandia pamoja na wizi wa tiketi.
Wambura alisema kuwa mfumo huo wa kuchukua tiketi katika mashine maalumu umeshafungwa kwenye viwanja vinane katika viwanja mbalimbali vya hapa nchini kama Kaitaba, Taifa, Mbeya, Azam, Mkwakwani, Arusha na Jamhuri.
Pia tiketi hizo zitapatikana kwenye huduma ya Max malipo.

0 comments:

Post a Comment