Facebook

Monday, 14 July 2014

Tetesi za Usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya.


Salim Kikeke's photo.
Arsenal wamepata matumaini zaidi ya kumsajili Sami Khedira, 27, baada ya kiungo huyo kukataa kusaini mkataba mpya na Real Madrid (Daily Star), 
 Salim Kikeke's photo.
Arsenal pia wapo katika mazungumzo ya kumsajili Loic Remy kwa pauni milioni 8 kutoka QPR iliyopanda daraja (Independent), 
 Salim Kikeke's photo.
Hata hivyo mazungumzo kati ya Arsenal na Remy yanadaiwa kuvunjika baada ya Remy kutokubali maslahi binafsi, huku Newcastle na Tottenham wakitaka kumchukua (Daily Mail),
 
 Chelsea wanataka pauni milioni 8 kwa ajili ya beki Ryan Bertrand, 24, ambaye ananyatiwa na Liverpool na Tottenham (Daily Express),
 
 Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Marouanne Chamakh, 30, amekubali mkataba wa miaka miwili kusalia Crystal Palace, huku akikubali kupunguziwa mshahara kiwango kikubwa (Guardian), 
 Salim Kikeke's photo.
Liverpool wameingia kwenye mbio sawa na Tottenham za kumsajili Wilfried Bony, 25, ambaye Swansea wanamuuza kwa pauni milioni 20 (Talksport), 
 
Lazio wanaamini wana kipaumbele zaidi kumsajili Stefan De Vrij, 22, kutoka Feyenoord, ambaye anasakwa pia na Manchester United (Daily Express),
 
 kiungo wa Spain Mikel Arteta, 32, hana nia ya kuhama Arsenal kwa mujibu wa wakala wake Inaki Ibanez (Times), 
 
Arsenal wana matumaini ya kukamilisha usajili wa Javi Manquillo kutoka Spain na Mathieu Debuchy, kuziba nafasi za Bacary Sagna na Carl Jenkinson (Daily Mail), 
 
Everton huenda wakamsajili Muhamed Besic, 21, raia wa Bosnia Herzegovina kwa euro milioni tano (Daily Mirror),
 
 kiungo wa Juventus amezua gumzo zaidi la kuhamia Chelsea baada ya kuonekana katika mitaa ya Stamford Bridge (Daily Mail), 
 
Manchester United huenda wakamfuatilia Ben Davies kuziba nafasi ya Patrice Evra (Daily Mail), 
 
Chelsea wamejiunga na Arsenal na Liverpool kumwania mshambuliaji wa Real Sociedad Antoine Griezman, 23 aliyekataa mkataba mpya (Daily Express),
 
Mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, anatazamiwa kwenda Juventus kwa pauni milioni 17.5. Real Madrid watakuwa na uwezo wa kumnunua tena baada ya mwaka mmoja kwa pauni milioni 23.8 (Daily Mail).
 
 Hizo ndio tetesi za leo, share na wapenda soka wote. Nyingine kesho tukijaaliwa. Chee

Related Posts:

  • Tetesi zote za Usajili wa wachezaji barani Ulaya siku ya leo.Dau la Manchester United la pauni milioni 110 kwa Real Madrid kumtaka Gareth Bale, 25 na beki Rafael Varane, 22 limekataliwa na klabu hiyo ya La Liga (Daily Express),   Real Madrid wana uhakika wa kumsajili kwa pauni m… Read More
  • Chelsea yarusha ndoano kwa Gundogan.Timu ya chelsea inatajwa katika mbio za kuhitaji saini ya mchezaji IIkay Gundogan kutoka Dortmund lakini taarifa zinasema mchezaji huyo yupo katika mazungumzo na vilabu vingine vya Barcelona, Manchester United.Bayern na Ars… Read More
  • Mbeya City yafungua ukurasa wa usajili.Mshambuliaji wa kutumainiwa wa Ndanda Fc, Gideon Benson amesaini kandarasi ya mwaka mmoja na nusu kujiunga na kikosi ch Mbeya City fc kinachonolewa na Juma Mwambusi katika msimu ujao Benson ameweka kando ofa kadhaa aliz… Read More
  • Benitez kutangazwa kocha mpya Real Madrid. Rafael Benitez anatarajiwa kutangazwa leo hii kuwa meneja mpya wa Real Madrid. Meneja huyo wa zamani wa Liverpool na Chelsea, aliyekuwa meneja wa Napoli msimu wa 2014-15 atachukua nafasi ya Carlo Ancelotti kwenye uwanja w… Read More
  • Singano "Messi" katika mtihani mzito Msimbazi. SIMBA SC inajipanga kumchukulia hatua mchezaji wake, Ramadhani Singano ‘Messi’ kwa kuituhumu klabu hiyo kughushi Mkataba wake. Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba SC, Hajji Sunday Manara ‘Zungu’ amefanya Mkut… Read More

0 comments:

Post a Comment