
Fifa imetangaza orodha ya majina 10 watakaowania tuzo ya mchezaji bora katika michuano ya Kombe la Dunia - 2014 Golden Ball.

Wachezaji watatu wametoka Argentina, Angel Di Maria, Javier Mascherano na Lionel Messi. Mahasimu wao wa siku ya Jumapili Ujerumani, imetoa wachezaji wanne, Mats Hummels, Toni Kroos, Phillip Lahm na Thomas Muller.
Wengine ni James Rodriguez kutoka Colombia, Neymar wa Brazil na Arjen Robben wa Uholanzi.


Washindi watatangazwa baada ya mchezo wa fainali siku ya Jumapili.
0 comments:
Post a Comment