Facebook

Monday, 14 July 2014

FIFA YATANGAZA WATAKAOWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA

Salim Kikeke's photo.
Fifa imetangaza orodha ya majina 10 watakaowania tuzo ya mchezaji bora katika michuano ya Kombe la Dunia - 2014 Golden Ball.
Salim Kikeke's photo.
Wachezaji watatu wametoka Argentina, Angel Di Maria, Javier Mascherano na Lionel Messi. Mahasimu wao wa siku ya Jumapili Ujerumani, imetoa wachezaji wanne, Mats Hummels, Toni Kroos, Phillip Lahm na Thomas Muller.
Wengine ni James Rodriguez kutoka Colombia, Neymar wa Brazil na Arjen Robben wa Uholanzi.
 
Salim Kikeke's photo. Fifa pia imetangaza majina ya watakaowania tuzo ya golikipa bora wa michuano hiyo. Keylor Navas wa Costa Rica, Manuel Neuer wa Ujerumani na Sergio Romero wa Argentina watawania tuzo hiyo.
Salim Kikeke's photo. Wakati huohuo Memphis Depay wa Uholanzi, Paul Pogba na Raphael Varane wa Ufaransa wamechaguliwa kuwania tuzo ya mchezaji bora chipukizi katika Kombe la Dunia.
Washindi watatangazwa baada ya mchezo wa fainali siku ya Jumapili.

Related Posts:

  • VAN GAAL :MOURINHO AMEJIJENGA MWENYEWE Meneja wa Manchester United Louis van Gaal amesisitiza kuwa hajafanya lolote kubwa kusababisha Jose Mourinho kuwa moja ya makocha wenye mafanikio duniani. Mourinho, ambaye ni meneja wa Chelsea kwa sasa, alifanya kazi chini y… Read More
  • Diego Costa hatihati. Diego Costa huenda akacheza katika mechi ya Ligi Kuu ya England dhidi ya Manchester United licha ya kuugua na kulazimika kupelekwa hospitali. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Spain, 26, amekuwa akipata nafuu akiwa nyumbani na … Read More
  • Manchester United yabanwa mbavu Ligi Kuu Uingereza.   Ligi kuu ya England imeendelea jana usiku ambapo Manchester United ilijikuta ikibanwa mbavu na kushindwa kufurukuta ugenini kwa West Bromwich Albion na kutoka sare ya mabao 2-2 licha kwamba ilitawala mc… Read More
  • Tanzania yaifumua Benin 4-1Taifa Stars imeitungua Benin kwa mabao 4-1 katika mechi ya kitarafiki ya kimataifa iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mabao ya Stars yalifungwa na wachezaji wake wawili wanaokipiga nchini na wawili w… Read More
  • Majeruhi wazidi kuongezeka Arsenal.   Kwa sasa tuna wachezaji kumi wa kikosi cha kwanza wapo nje kwa majeruhi. Katika mchezo wa jana wa timu ya taifa Uingereza kufuzu Euro 2016 Danny Welbeck alitonesha enka yake na kutolewa nje dakika 10 kabla ya mpi… Read More

0 comments:

Post a Comment