Facebook

Thursday, 3 July 2014

Barcelona wameanza mazungumzo na Liverpool ili kumsajili Luis Suarez.

 Photo: BARCA WAANZA MAZUNGUMZO NA LIVERPOOL KUMSAJILI SUAREZ
Barcelona wataanza mazungumzo na Liverpool siku ya Jumatano (Leo) kuhusiana na uhamisho wa Luis Suarez.
Maafisa kutoka klabu hizo mbili watakutana London kujadili mkataba wa mshambuliaji huyo raia wa Uruguay. Suarez, ambaye amesalia na miaka minne kwenye mkataba wake na Liverpool, anatumikia adhabu ya miezi minne kwa kumng'ata Georgio Chiellini wa Italy wakati wa Kombe la Dunia. Liverpool huenda wakakubali kitita cha pauni milioni 80 kwa ajili ya Suares, ambaye alijiunga na Liverpool kutoka Ajax kwa pauni milioni 22.7 mwaka 2011. Hata hivyo inaaminika kuwa Barcelona wanataka kutoa karibu pauni milioni 60. Mkataba wowote huenda ukategemea iwapo Barcelona itamtoa Alexis Sanchez kama sehemu ya kumchukua Suarez.
 Barcelona wataanza mazungumzo na Liverpool siku ya Jumatano (Leo) kuhusiana na uhamisho wa Luis Suarez.
Maafisa kutoka klabu hizo mbili watakutana London kujadili mkataba wa mshambuliaji huyo raia wa Uruguay. Suarez, ambaye amesalia na miaka minne kwenye mkataba wake na Liverpool, anatumikia adhabu ya miezi minne kwa kumng'ata Georgio Chiellini wa Italy wakati wa Kombe la Dunia.
   Liverpool huenda wakakubali kitita cha pauni milioni 80 kwa ajili ya Suares, ambaye alijiunga na Liverpool kutoka Ajax kwa pauni milioni 22.7 mwaka 2011. Hata hivyo inaaminika kuwa Barcelona wanataka kutoa karibu pauni milioni 60. Mkataba wowote huenda ukategemea iwapo Barcelona itamtoa Alexis Sanchez kama sehemu ya kumchukua Suarez.
 
Endelea kutembelea www.bantutz.com uweze kupata taarifa zote zitakazokuwa zinahusiana na usajili katika kipindi hiki cha uasajili barani Ulaya.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment