Facebook

Monday, 7 July 2014

Di Maria "sina shaka kuhusu nusu fainali"


Mchezaji kiungo cha kati wa Argentina,Angel Di Maria ana shaka ikiwa atashiriki mechi ya nusu fainali Jumatano ijayo kati ya Argentina na Uholanzi.
Hi ni baada ya mchezaji huyo kupata jeraha la Paja wakati wa mechi yao dhidi ya Ubelgiji ambapo walishinda bao moja bila.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, alilazimika kupumzika baada ya dakika 33 ya kipindi cha kwanza cha mechi nchini Brasilia baada ya kujeruhiwa alipokuwa anapiga shuti.
Kocha Alejandro Sabella alinukuliwa akisema: "Angel ana tatizo la Paja lake la kulia na kwamba atachunguzwa zaidi.
Di Maria aliingiza bao la ushindi katika mechi yao dhidi ya Switzerland katika awamu ya muondoano.
Enzo Perez wa Benfica alichukua nafasi yake katika mechi dhidi ya Ubelgiji.

Related Posts:

  • Sababu ya Ronaldinho Kutojiunga Man Utd na Kutimkia Barca hii hapa.   Ronaldinho "mtu mmoja tu ndiye aliye ni fanya nisijiunge na Man united sio Sir Alex" Man united ilikua ikamilishe usajili wa kiungo Ronaldinho Gaúcho ndani ya masaa 48 lakini akatokea mtu akawanyang'anya tonge md… Read More
  • Fellaini "Sina cha kuonyesha Man Utd"   kiungo wa Man united Marouane Fellaini amesema hana cha kuonyesha Man united. Mchezaji huyo alie sajiliwa kwa dau la paundi milioni 27 toka timu ya Evarton na kocha David Moyes amekua akitawaliwa na kiwango c… Read More
  • Zifahamu ziara za Manchester United.   Manchester United watakwenda nchini Marekani ikiwa ni ziara yao kwa mechi za majaribio kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Uingereza. Tarehe 23 mwezi huu dhidi ya LA Galaxy Tarehe 26 mwezi huu dhidi ya… Read More
  • Jezi mpya za United zavuja Man United wanakuja na kocha mpya, jezi mpya zikiwa na mdhamini mpya Chevrolet. Fulana mpya za Manchester United watakazovaa wakiwa nyumbani zimevuja mtandaoni – picha mpya za fulana hizo… Read More
  • Van Gaal aeleza sababu za kubadili kipa.   Kocha wa Uholanzi Luis van Gaal amesema urefu wa kipa Tim Krul ndio ulimfanya amchezeshe katika mikwaju ya penati katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Costa Rica. Krul, mwenye urefu wa futi 6 na inchi 4, (mi… Read More

0 comments:

Post a Comment