Facebook

Monday, 7 July 2014

Di Maria "sina shaka kuhusu nusu fainali"


Mchezaji kiungo cha kati wa Argentina,Angel Di Maria ana shaka ikiwa atashiriki mechi ya nusu fainali Jumatano ijayo kati ya Argentina na Uholanzi.
Hi ni baada ya mchezaji huyo kupata jeraha la Paja wakati wa mechi yao dhidi ya Ubelgiji ambapo walishinda bao moja bila.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, alilazimika kupumzika baada ya dakika 33 ya kipindi cha kwanza cha mechi nchini Brasilia baada ya kujeruhiwa alipokuwa anapiga shuti.
Kocha Alejandro Sabella alinukuliwa akisema: "Angel ana tatizo la Paja lake la kulia na kwamba atachunguzwa zaidi.
Di Maria aliingiza bao la ushindi katika mechi yao dhidi ya Switzerland katika awamu ya muondoano.
Enzo Perez wa Benfica alichukua nafasi yake katika mechi dhidi ya Ubelgiji.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment