Facebook

Wednesday, 9 July 2014

Polisi amuua kobe kwa kumpiga risasi Uganda.

Photo: POLISI AUA KOBE UGANDA
Polisi mmoja nchini Uganda imeripotiwa amempiga risasi na kumuua kobe mmoja baada ya kudai "alishambuliwa vikali" na mnyama huyo.
Tukio hilo lilitokea katika wilaya ya Nebbi, kaskazini mwa Uganda karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. kwa mujibu wa gazeti la New Vision afisa huyo, Charles Onegiu alisema kobe huyo aliingia nyumbani kwake na kumshambulia wakati akiwa amekaa anakunywa chai. "Nilijaribu kumtisha, lakini kobe huyo akawa mkali sana. Nilichukua fimbo na kumfukuza, lakini badala yake akaanza ghasia," polisi huyo ameliambia New Vision. Baada ya kujaribu kumfukuza kwa kutumia kiti cha plastiki, amesema alitoa bunduki yake na kumpiga risasi. Kundi moja la kidini lilimuombea afande Onegiu kabla ya kumchoma moto kobe. Kamanda wa polisi wa wilaya ya Nebbi Onesmus Mwesigwa alipoulizwa kuhusu jambo hilo amesema huenda shambulio hilo limetokana na imani za kishirikina, akisema watu hufikiri "kuna mtu ananitafuta". Kamanda Mwesigwa amewataka wananchi wa eneo hilo kuwa watulivu, limesema New Vision.

Polisi mmoja nchini Uganda imeripotiwa amempiga risasi na kumuua kobe mmoja baada ya kudai "alishambuliwa vikali" na mnyama huyo.
Tukio hilo lilitokea katika wilaya ya Nebbi, kaskazini mwa Uganda karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. kwa mujibu wa gazeti la New Vision afisa huyo, Charles Onegiu alisema kobe huyo aliingia nyumbani kwake na kumshambulia wakati akiwa amekaa anakunywa chai. 
 "Nilijaribu kumtisha, lakini kobe huyo akawa mkali sana. Nilichukua fimbo na kumfukuza, lakini badala yake akaanza ghasia," polisi huyo ameliambia New Vision. Baada ya kujaribu kumfukuza kwa kutumia kiti cha plastiki, amesema alitoa bunduki yake na kumpiga risasi. Kundi moja la kidini lilimuombea afande Onegiu kabla ya kumchoma moto kobe. 
 
 Kamanda wa polisi wa wilaya ya Nebbi Onesmus Mwesigwa alipoulizwa kuhusu jambo hilo amesema huenda shambulio hilo limetokana na imani za kishirikina, akisema watu hufikiri "kuna mtu ananitafuta". Kamanda Mwesigwa amewataka wananchi wa eneo hilo kuwa watulivu, limesema New Vision.

Related Posts:

  • Polisi Polisi wa Ufaransa matatani kwa ubaguzi wa Rangi.! Mzozo wa ubaguzi wa rangi unatokota nchini Ufaransa baada ya picha kupatikana za maafisa wa polisi wazungu wakiwa wamejipaka rangi nyeusi huku wakiiga mienendo ya nyani katika sherehe moja. Mkuu wa polisi wa Ufarans… Read More
  • Paka mzee zaidi duniani afariki.! Paka aliyekuwa akitambulika rasmi kuwa ndio mzee zaidi duniani kwa sasa, amefariki dunia akiwa na miaka 24. Paka huyo aitwaye Poppy alizaliwa mwezi Februari mwaka 1990, mwezi ambao Nelson Mandela alitoka gerezani-, na al… Read More
  • Unamjua mwanaume mwenye uume mkubwa zaidi duniani.? Mfuatilie hapa Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 41 sasa katika mahojiano yake na The Huffington alisema kwamba huwa anapata shida sana masecurity anapokua kwenye airport anapotaka kusafiri kwani humsumbua sana.   Anasema “ili… Read More
  • Nguruwe mwenye akili,atoroka kuchinjwa.  Nguruwe huyu mdogo hakuwa na nia kabisa ya kufika sokoni kwa ajili ya kuuzwa na kuchinjwa na badala yake akaamua kutumia mbinu mbadala kutoroka kutoka kwenye gari iliyokuwa inatembea. Nguruwe huyo alirekodiwa na ka… Read More
  • mwanamke ajifungua mjusi.Indonesia. Mwanamke mmoja nchini Indonesia amejifungua mjusi badala ya mtoto. Mwanamke huyo Debi Nubatonis, mwenye umri wa miaka 31, ameanza kupata vitisho kutoka kwa kundi la vijana kutokana na kitendo hicho wakimtuhumu kwa uchawi… Read More

0 comments:

Post a Comment