Facebook

Wednesday, 9 July 2014

Polisi amuua kobe kwa kumpiga risasi Uganda.

Photo: POLISI AUA KOBE UGANDA
Polisi mmoja nchini Uganda imeripotiwa amempiga risasi na kumuua kobe mmoja baada ya kudai "alishambuliwa vikali" na mnyama huyo.
Tukio hilo lilitokea katika wilaya ya Nebbi, kaskazini mwa Uganda karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. kwa mujibu wa gazeti la New Vision afisa huyo, Charles Onegiu alisema kobe huyo aliingia nyumbani kwake na kumshambulia wakati akiwa amekaa anakunywa chai. "Nilijaribu kumtisha, lakini kobe huyo akawa mkali sana. Nilichukua fimbo na kumfukuza, lakini badala yake akaanza ghasia," polisi huyo ameliambia New Vision. Baada ya kujaribu kumfukuza kwa kutumia kiti cha plastiki, amesema alitoa bunduki yake na kumpiga risasi. Kundi moja la kidini lilimuombea afande Onegiu kabla ya kumchoma moto kobe. Kamanda wa polisi wa wilaya ya Nebbi Onesmus Mwesigwa alipoulizwa kuhusu jambo hilo amesema huenda shambulio hilo limetokana na imani za kishirikina, akisema watu hufikiri "kuna mtu ananitafuta". Kamanda Mwesigwa amewataka wananchi wa eneo hilo kuwa watulivu, limesema New Vision.

Polisi mmoja nchini Uganda imeripotiwa amempiga risasi na kumuua kobe mmoja baada ya kudai "alishambuliwa vikali" na mnyama huyo.
Tukio hilo lilitokea katika wilaya ya Nebbi, kaskazini mwa Uganda karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. kwa mujibu wa gazeti la New Vision afisa huyo, Charles Onegiu alisema kobe huyo aliingia nyumbani kwake na kumshambulia wakati akiwa amekaa anakunywa chai. 
 "Nilijaribu kumtisha, lakini kobe huyo akawa mkali sana. Nilichukua fimbo na kumfukuza, lakini badala yake akaanza ghasia," polisi huyo ameliambia New Vision. Baada ya kujaribu kumfukuza kwa kutumia kiti cha plastiki, amesema alitoa bunduki yake na kumpiga risasi. Kundi moja la kidini lilimuombea afande Onegiu kabla ya kumchoma moto kobe. 
 
 Kamanda wa polisi wa wilaya ya Nebbi Onesmus Mwesigwa alipoulizwa kuhusu jambo hilo amesema huenda shambulio hilo limetokana na imani za kishirikina, akisema watu hufikiri "kuna mtu ananitafuta". Kamanda Mwesigwa amewataka wananchi wa eneo hilo kuwa watulivu, limesema New Vision.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment