Facebook

Wednesday, 9 July 2014

Rais wa Brazil awataka wananchi kuwa "Ngangari"

Salim Kikeke's photo.


Rais wa Brazil Dilma Rousselff ameitaka nchi yake 'kujinyanyua' baada ya kichapo cha mabao 7-1 dhidi ya Ujerumani katika Kombe la Dunia.

Salim Kikeke's photo.
"Kama Wabrazil wote, nimesikitishwa sana sana baada ya kufungwa. Lakini hatutosononeka," rais huyo ame - tweet.
Kocha wa Brazil Luiz Filipe Scolari amesema kupoteza mchezo huo ilikuwa "siku yake mbaya zaidi maishani mwake".

Salim Kikeke's photo. Vyombo vya habari vya Brazil vimeandika habari za jinsi watu walivyopokea mshtuko huo wa matokeo siku ya Jumatano, vikieleza matokeo hayo kuwa ni "udhalilishwaji wa kihistoria". Matokeo hayo ni mabaya zaidi katika historia ya Brazil katika Kombe la Dunia.

Endelea kutembelea www.bantutz.com kupata habari mbalimbali kwa muda na wakati muafaka.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment