Facebook

Thursday, 10 July 2014

Ushindi wa Ujerumani wavunja rekodi za Twitter.

Photo: USHINDI WA UJERUMANI WAVUNJA REKODI ZA TWITTER
Ushindi wa Ujerumani wa 7-1 dhidi ya Brazil katika nusu fainali ya Kombe la Dunia umekuwa gumzo kubwa. Mchezo huo umekuwa jambo la kimichezo lililojadiliwa zaidi kwenye mtandao wa Twitter mpaka sasa. Takriban tweets milioni 35.6 zilitumwa katika kipindi cha dakika 90 za mchezo huo, na kuvunja rekodi ya dunia. Pia ilivunja rekodi ya tweets kutumwa katika dakika moja, ambapo goli la tano lilisababisha tweets 580,601 kutumwa katika muda wa dakika moja tu. Tweets sita kati ya kumi zilizokuwa zikirindima zaidi zilikuwa zinataja mechi hiyo, huku #BrazilvsGermany ikirindima zaidi. Miroslav Klose (kwenye picha) ndio alikuwa mchezaji aliyetajwa zaidi katika twitter, akifuatiwa na Toni Kroos. Julio Cesar, Oscar na Fred ndio wachezaji wa Brazil waliotajwa zaidi. Rekodi ya zamani ya shughuli ya kimichezo ilikuwa katika mechi kati ya Brazil na Chile, ambapo tweets 389,000 zilitumwa katika kipindi cha dakika moja. 
 Ushindi wa Ujerumani wa 7-1 dhidi ya Brazil katika nusu fainali ya Kombe la Dunia umekuwa gumzo kubwa. Mchezo huo umekuwa jambo la kimichezo lililojadiliwa zaidi kwenye mtandao wa Twitter mpaka sasa. 
  Takriban tweets milioni 35.6 zilitumwa katika kipindi cha dakika 90 za mchezo huo, na kuvunja rekodi ya dunia. Pia ilivunja rekodi ya tweets kutumwa katika dakika moja, ambapo goli la tano lilisababisha tweets 580,601 kutumwa katika muda wa dakika moja tu. 
       Tweets sita kati ya kumi zilizokuwa zikirindima zaidi zilikuwa zinataja mechi hiyo, huku #BrazilvsGermany ikirindima zaidi. Miroslav Klose (kwenye picha) ndio alikuwa mchezaji aliyetajwa zaidi katika twitter, akifuatiwa na Toni Kroos. 
Julio Cesar, Oscar na Fred ndio wachezaji wa Brazil waliotajwa zaidi. Rekodi ya zamani ya shughuli ya kimichezo ilikuwa katika mechi kati ya Brazil na Chile, ambapo tweets 389,000 zilitumwa katika kipindi cha dakika moja.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment