Facebook

Wednesday, 16 July 2014

Israel yakubali pendekezo la Misri juu ya Gaza.


 Photo: ISRAEL YAKUBALI PENDEKEZO LA MISRI JUU YA GAZA
Israel imekubali pendekezo la Misri la kutuliza mapigano katika mzozo wa Gaza.
Hamas, inayodhibiti Gaza haijajibu rasmi, lakini tawi lake la kijeshi limetupilia mbali mpango huo likisema ni kama "kujisalimisha".
Chini ya mpango huo, mapigano yatasitishwa mara moja, na kufuatiwa na mfululizo wa mazungumzo ya ngazi ya juu mjini Cairo na wajumbe kutoka pande zote mbili.
Maafisa wa Palestina wanasema watu wasiopungua 192 wameuawa na mashambulio ya anga ya Israel yaliyoanza siku nane zilizopita, kuzuia maroketi yanayoelekezwa Israel.
Kumekuwa hakuna mashambulio ya anga kutoka Israel kwenda Gaza tangu saa tatu asubuhi saa za huko ambao ni muda uliopendekezwa wa kusimamisha mapigano, lakini kumekuwa na roketi moja iliyorushwa kwenda Israel.

Israel imekubali pendekezo la Misri la kutuliza mapigano katika mzozo wa Gaza.
Hamas, inayodhibiti Gaza haijajibu rasmi, lakini tawi lake la kijeshi limetupilia mbali mpango huo likisema ni kama "kujisalimisha".
Chini ya mpango huo, mapigano yatasitishwa mara moja, na kufuatiwa na mfululizo wa mazungumzo ya ngazi ya juu mjini Cairo na wajumbe kutoka pande zote mbili.
Maafisa wa Palestina wanasema watu wasiopungua 192 wameuawa na mashambulio ya anga ya Israel yaliyoanza siku nane zilizopita, kuzuia maroketi yanayoelekezwa Israel.
Kumekuwa hakuna mashambulio ya anga kutoka Israel kwenda Gaza tangu saa tatu asubuhi saa za huko ambao ni muda uliopendekezwa wa kusimamisha mapigano, lakini kumekuwa na roketi moja iliyorushwa kwenda Israel.

Related Posts:

  • Mabaki ya ndege Algeria yaonekana Mabaki ya ndege iliyopotea ikiwa na watu 116 njiani kutoka Burkanafaso kwenda Algers yamepatikana nchini Mali. Maafisa wa Jeshi wa Burkina faso wamesema ndege hiyo iliyokuwa chini ya shirika la ndege la Algeria imeang… Read More
  • Juhudi za kutafuta amani Gaza zaingia dosari. Wapalestina zaidi ya 800 wameuawa na Waisraeli 35 Israeli imeendelea kuivirumishia makombora Gaza kucha kutwa ,huku kikao cha mawaziri wa baraza la Usalama kikitarajiwa huko Marekani kujadili mapendekezo mapya ya … Read More
  • Mama anayeugua Ebola atoroshwa Mwanamke aliyeambukizwa Ebola atoroshwa Hospitalini huko Freetown Hali ya Tahadhari imetangazwa mjini Freetown Sierra Leone baada ya mwanamke mmoja aliyeambukizwa Ebola kutoroshwa kutoka Hospitalini na jamaa zake kw… Read More
  • Air Algerie AH5017: Abiria wote waliaga Abiria wote wa ndege ya Air Algerie waliangamia jangwani Abiria wote na wahudumu wa ndege ya Air Algerie AH5017 waliangamia jangwani. Rais wa Ufaransa Francois Hollande ametangaza kuwa majeshi … Read More
  • Maandamano yazuka Palestina polisi wakabiliana na raia Palestina Maandamano makubwa yamefanyika katika ukingo wa Magharibi mwa Palestina karibu na mpaka wake na Israel kupinga mashambulio yanayofanywa na Israel. Waandamanaji hao wakiwa na hasi… Read More

0 comments:

Post a Comment