Facebook

Friday, 4 July 2014

Tetesu za Usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya.

Salim Kikeke's photo.Salim Kikeke's photo.Salim Kikeke's photo.
 
Mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake wa pauni milioni 80 kwenda Barcelona katika saa 48 zijazo (Daily Mail),
 
 Dau la Liverpool la pauni milioni 20 la kumtaka beki Dejan Lovren limekataliwa na Southampton (Liverpool Echo), 
 
Manchester United wamepewa Angel Di Maria na Real Madrid kwa pauni milioni 40. Arsenal, Paris St-Germain na Juventus pia wanamtaka pia mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina (Daily Star),
 
 Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger ana uhakika wa kuwasajili Alexis Sanchez na Mathieu Debuchy kwa pauni milioni 35 (Daily Mirror),
 
Washika bunduki hao pia watatoa dau la pauni milioni 20 kwa Southampton kumsajili Morgan Schneiderlin, ambaye anasakwa pia na Napoli (Daily Express),
 
 Bayern Munich huenda wakawazidi kete Manchester United, Liverpool na Arsenal kumchukua winga wa Fiorentina, Juan Cuadrado (Daily Express),
 
 Arsenal pia wametoa dau la pauni milioni 23.8 kumwania kiungo wa Real Madrid, Sami Khedira na watamtumia rafiki yake wa karibu Mesut Ozil kumshawishi (Metro), 
 
Dau la pauni milioni 32 la Manchester City kumtaka beki Eliaquim Mangala limekubaliwa na Porto, lakini bado wanasubiri kama Chelsea nao pia watapanda dau (Daily Star), 
 
Juventus wako makini kumsajili beki wa Manchester United Patrice Evra, ambaye amesaini mkataba mpya Old Trafford mwezi uliopita (Talksport), 
 
Barcelona wataajiri mwanasaikolojia wa kumsaidia Luis Suarez kukabiliana na 'mizimu' atakapokamilisha uhamisho wake (Sun)
 
 QPR wanatarajia kukamilisha usajili wa Rio Ferdinand wiki ijayo (Get WestLondon),
 
kipa wa Chelsea Petr Cech huenda akaondoka Darajani kabla ya msimu mpya kuanza, kwa mujibu wa wakala wake (Talksport). 
 
Share tetesi hizi na wapenda soka wote. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.
 
Endelea kutembelea www.bantutz.com uweze kupata tetesi mbalimbali za usajili kutoka katika vyanzo mbalimbali sisi tutakukusanyia na utapata tetesi zote hapa kwa muda na wakati muafaka.

Related Posts:

  • Tetesi za Usajili barani Ulaya. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anafikiria kumsaini striker wa AC Milan Mario Balotelli baada ya mchezaji huyo kuambiwa hahitajiki tena San Siro (Daily Mirror), Liverpool, Chelsea na Tottenham pia zinaweza kumfuatilia… Read More
  • Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya.   Chelsea watajaribu kumsajili kiungo wa Barcelona Cesc Fabegas kuziba nafasi ya Frank Lampard (Daily Telegraph),    Nyota wa zamani wa Liverpool Robbie Fowler amemsihi Brendan Rodgers kumsajili Fabreg… Read More
  • David Villa na Frank Lampard wamejiunga na New York FC David Villa na Frank Lampard wamejiunga na New York FC inayoshiriki ligi ya Marekani - timu hiyo inamilikiwa na mmiliki wa Manchester City Sheikh Mansour. Wachezaji hawa wawili leo walionekana katika hospital ya Bri… Read More
  • Arsene Wenger azidi kumuwinda Mario Balotelli   Kocha Arsene Wenger yuko kwenye mbio za kumuwania Mario Balotelli.Timu ya AC Milan wako mbioni kutua mzigo huo wa zamani wa Manchester City kwenye kipindi hiki cha jua, Arsenal wameshapaza sauti. Meneja wa washika… Read More
  • Tetesi za usajili barani Ulaya.   Manchester United imekwisha fahamu wachezaji watano inayowataka, na meneja mpya Louis van Gaal atapewa paundi milioni 220 kuwapata. Van Gaal anataka kumchukua kiungo Kevin Strootman kutoka Roma ya Italia (Dail… Read More

0 comments:

Post a Comment