Miwani ya kisasa ya Google imedukuliwa, ambapo sasa inaweza kufanya kazi kwa kusoma mawazo ya mtu.
Mtumiaji anaweza kupiga picha kwa kufikiria tu.
Kwa kutumia miwani hiyo ya kisasa na kuunganisha kichwani na kifaa kijulikanacho kama electroencephalography (EEG) ambapo kifaa uroro huweza kusoma unachofikiria, na hata kupiga picha bila kujigusa au kubonyeza mahala popote.
Kampuni ya This Place ya London
iliyotengeneza kifaa uroro hicho (software) imesema inaweza kutumika
pale watu wanapohitaji kufanya mambo mengine bila kutumia mikono yao,
mathalan wakati madaktari wanafanya upasuaji.
This Place imetoa kifaa uroro hicho MindRDR bure na wana imani kuwa huenda wataalam wengine wanaweza kutumia kwa shughuli nyingine.
This Place imetoa kifaa uroro hicho MindRDR bure na wana imani kuwa huenda wataalam wengine wanaweza kutumia kwa shughuli nyingine.
Hata hivyo Google imesema haitambui kifaa uroro hicho.
"Miwani yetu ya Google haiweza kusoma mawazo ya mtu" msemaji wa Google amesema.
Kutaka kujaribu kifaa uroro hicho kama una miwani ya Google, ingia:hapa
"Miwani yetu ya Google haiweza kusoma mawazo ya mtu" msemaji wa Google amesema.
Kutaka kujaribu kifaa uroro hicho kama una miwani ya Google, ingia:hapa
0 comments:
Post a Comment