Facebook

Thursday, 10 July 2014

AL Shabaab washambulia ikulu Somalia

wapiganaji wa AL shabaab
Vikosi vya serikali Somalia vimefanikiwa kuidhibiti upya ikulu ya rais katika mji mkuu Mogadishu baada ya hapo awali wapiganaji wa kiislamu kuishambulia.
Maafisa wanasema washambuliaji wapatao watano kutoka kundi la al-Shabab - waliuawa walipoingia katika eneo la ikulu hiyo.
Washambuliaji hao wanadaiwa kulipua bomu lililotegwa kwenye gari karibu na langu kuu la Ikulu hiyo.
waziri wa habari wa Somalia Mustaf Dhuhulow
Waziri wa habari na mawasiliano wa Somalia Mustaf Dhuhulow amesema kuwa tayari mmoja wa washambuliaji hao amekamatwa na anahojiwa na polisi.
Waziri Mustaf amesema, '' Walishambulia ikulu ya rais saa za jioni. Alikuwa watu washambuliaji watatu pamoja na dereva wao. Washambuliaji hao waliuawa lakini dereva wao alipata majeraha madogo na anazuiliwa na polisi na kuhojiwa. Walijaribu kuvamia Villa Somalia lakini wakakomeshwa. Tutawapa maelezo zaidi baadaye. Na tutaweza kutoa maelezo zaidi kwa raia wa Somalia na dunia nzima.''
Shambulio la Al shabaab Mogadishu
Hii ni mara ya pili kwa Al Shabaab kuvamia ikulu ya rais mjini Mogadishu mwaka huu japo mara ya kwanza walifanikiwa kuingia ndani.
Rais Hassan Sheikh Mohamoud hakuwepo wakati wa shambulio hilo.
Kundi la wapiganaji wa kiislamu Al shabaab limefukuzwa kutoka mjini Mogadishu tangu mwaka wa 2011 lakini limekuwa likifanya mashambulio ya kuvizia tangu wakati huo.
Wanamgambo hao wanaaminiwa kufanya mashambulio kadhaa pia katika nchi jirani ya Somalia kama vile Kenya, Uganda na Tanzania kama njia ya kulipiza kisasi kwa kuingia majeshi ya Umoja wa Afrika nchini Somalia.

Related Posts:

  • Mabaki ya ndege Algeria yaonekana Mabaki ya ndege iliyopotea ikiwa na watu 116 njiani kutoka Burkanafaso kwenda Algers yamepatikana nchini Mali. Maafisa wa Jeshi wa Burkina faso wamesema ndege hiyo iliyokuwa chini ya shirika la ndege la Algeria imeang… Read More
  • Juhudi za kutafuta amani Gaza zaingia dosari. Wapalestina zaidi ya 800 wameuawa na Waisraeli 35 Israeli imeendelea kuivirumishia makombora Gaza kucha kutwa ,huku kikao cha mawaziri wa baraza la Usalama kikitarajiwa huko Marekani kujadili mapendekezo mapya ya … Read More
  • Maandamano yazuka Palestina polisi wakabiliana na raia Palestina Maandamano makubwa yamefanyika katika ukingo wa Magharibi mwa Palestina karibu na mpaka wake na Israel kupinga mashambulio yanayofanywa na Israel. Waandamanaji hao wakiwa na hasi… Read More
  • Mama anayeugua Ebola atoroshwa Mwanamke aliyeambukizwa Ebola atoroshwa Hospitalini huko Freetown Hali ya Tahadhari imetangazwa mjini Freetown Sierra Leone baada ya mwanamke mmoja aliyeambukizwa Ebola kutoroshwa kutoka Hospitalini na jamaa zake kw… Read More
  • Air Algerie AH5017: Abiria wote waliaga Abiria wote wa ndege ya Air Algerie waliangamia jangwani Abiria wote na wahudumu wa ndege ya Air Algerie AH5017 waliangamia jangwani. Rais wa Ufaransa Francois Hollande ametangaza kuwa majeshi … Read More

0 comments:

Post a Comment