Facebook

Monday, 24 November 2014

Njama ya polisi kumvua mwanamke Nguo yatibuka-Kenya

Afisa mmoja wa polisi wa utawala nchini
Kenya ni miongoni mwa wanaume
waliokamatwa kwa kujaribu kumvua nguo
mwanamke katika mtaa wa Komarock
viungani mwa mji mkuu Nairobi.
Polisi walisema watu wanne walimsingira
mwanamke huyo alipokuwa anaenda nyumbani
kutoka kanisani akiwa ameandamana na rafiki
yake.

Wanaume hao walijaribu kumvua nguo mmoja
wa wanawake hao ila waliokolewa na wananchi
waliokuwa wakielekea makwao.
Wanaume wawili waliokuwa wanawaokoa
wanawake hao walijeruhiwa.

Kwa mujibu wa taarifa za mtandao wa Daily
Nation, Kioo cha basi iliyokuwa barabarani pia
kilivunjika katika purukushanio hilo.
Polisi waliofika katika eneo la tukio waligundua
kuwa mmoja wa waliowashambulia wanawake
hao alikuwa afisa wa polisi.

Tukio hilo limefanyika siku chache tu baada ya
mamia ya wanawake kuandamana mjini Nairobi
kulaani kitendo cha kumvua mwanamke mmoja
mavazi yake yakisemekana kutokuwa na
heshima.

Related Posts:

  • HATIMAYE KIONGOZI WA AL SHABAB AUAWA Aliyekua kiongozi mkuu wa Alshabab Ahmed Abdi Godane ameripotiwa kuuawa!! Habari kutoka katika idara kuu ya ulinzi ya marekani PENTAGONI imesema kua kuuawa kwa kiongozi huyo mwanzilishi wa kikundi ambacho kimekua mwiba mkali… Read More
  • Boko Haram wazuia watu kuzika maiti Wapiganaji wa Boko Haram wamesababisha maafa Kaskazini ya Nigeria ngome yao ya vita Taarifa za kutisha zimeibuka kutoka mjini Bama moja… Read More
  • Mafuriko yaua nchini India Watu kadhaa wanahofiwa kufa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kuchukuliwa na maji katika jimbo la Kashmir nchini India. Basi hilo … Read More
  • KESI YA KENYATTA YAPIGWA KALENDAWaendesha mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya ICC iliyopo The Hague wameomba kesi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kuahirishwa tena. Bwana Kenyatta anashtakiwa kwa makosa dhidi ya ubinaadam, lakini upande wa mashtaka umes… Read More
  • Al-Qaeda yafungua tawi jipya India Kiongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda, Ayman al-Zawahiri amesema kuwa wamefungua tawi jipya la mtandao huo wa kigaidi nchini India i… Read More

0 comments:

Post a Comment