Facebook

Wednesday 29 April 2015

Borussia Dortmund watinga fainali baada ya kuifunga Bayern Munich.

Borussia Dortmund imetinga Fainali ya Kombe la ujerumani (DFB-
POKAL)baada ya kuwabwaga Mabingwa Watetezi Bayern Munich kwa
Penati 2-0 kufuatia Sare ya Bao 1-1 katika Dakika 120 za mchezo
uliopigwa Allianz Arena.
Borussia Dortmund itacheza na Mshindi wa Nusu Fainali nyingine
inayochezwa Leo kati ya Timu ya Daraja la 3 Arminia Bielefeld na
Klabu ya VfL Wolfsburg.
Katika Nusu Fainali hii, Bayern walitangulia kufunga Bao la Dakika
ya 29 la Robert Lewandowski na Dortmund kurudisha Dakika ya 75
kwa Bao la mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang.
Katika Dakika za Nyongeza 30, Dortmund walibaki Mtu 10 baada ya
Mchezaji wao Kampl kupewa Kadi Nyekundu lakini mwisho Bao zilibaki
1-1.
Kwenye Mikwaju Mitano ya Penati, Bayern walikosa Penati zao zote 4
zilizopigwa na Xabi Alonso, Philipp Lahm, Mario Gotze na Kipa Manuel
Neuer huku Dortmund wakifunga 2 kupitia Sebastian Kehl na Ilkay
Gundogan.

0 comments:

Post a Comment