Facebook

Wednesday 29 April 2015

Pacquiao atamba kumchakaza Mayweather

Zikiwa zimesalia siku chache kabla ya dunia kushuhudia mpambano wa
karne wa mabondia Floyd Mayweather na Manny Pacquiao,Bondia wa
Ufilipino Manny Pacquiao ametamba kumchakaza mpinzani wake
kwenye mpambano utakaofanyika Mei 2 mwaka huu katika ukumbi wa
Mgm Grand Vegas
Akiwa amezungukwa na mamia ya washabiki wake Pacquiao aliwaeleza
"msiwe na wasiwasi mimi ndie ninae pigana na nina uhakika asilimia
mia moja wa kushinda".
"Naamini huu ndio muda wa Mayweather kupoteza mchezo kwa mara
ya kwanza’’
Floyd Mayweather hajawahi poteza mchezo katika mapambano 47
aliyokwisha cheza ,Huku Pacquiao akiwa kapoteza mapambano 5 na
kutoka sare mara 2 katika mapambano 64 aliyocheza.

0 comments:

Post a Comment