Facebook

Wednesday 8 April 2015

COPA ITALIA : JUVE WAINYUKA FIORENTINA 3-0, HAO FAINALI !!

Wakicheza Ugenini bila ya Nyota wao bora,
Andrea Pirlo , Paul Pogba na Carlos Tevez,
Juventus , chini ya Kocha Massimiliano
Allegri, Usiku huu wameipindua kipigo cha
mechi ya kwanza na kuichapa Fiorentina
3-0 na kutinga Fainali ya Coppa Italiana.

Hii ni nafasi murua kwa Juve kutwaa Dabo
Msimu huu kwani kwenye Ligi Serie A wao
ndio Vinara wakiwa Pointi 14 mbele .

Bao za Juve, ambao walifungwa 2- 1 katika
Mechi ya kwanza zilifungwa na Alessandro
Matri , Roberto Pereyra na Leonardo
Bonucci.

0 comments:

Post a Comment