Facebook

Wednesday 29 April 2015

Barcelona wazidi "kuchanja mbuga" La Liga.

Vinara wa La Liga FC Barcelona Jana Usiku wameishindilia Getafe
Bao 6-0 na kupanda kuwa mbele ya Timu ya Pili Real Madrid kwa
Pointi 5.
Mabao ya Barca yalifungwa na mshambuliaji wao hatari Lionel Messi
aliyefunga mara mbili huku, Luis Suarez nae akitupia kambani mabao
mawili , Neymar na Xavi wakifunga bao moja moja.
Mabao hayo ya washambuliaji wa Barca, Messi, Suarez na Neymar
yamewafikisha zaidi ya mabao 100, kwa Msimu huu.
Hii Leo, Real Madrid walioko nafasi ya pili watakua na kibarua cha
kupetetana na Almeria Uwanjani Santiago Bernabeu.
Vita ya kuwania kiatu cha mfungaji bora kiko kwa Cristiano Ronaldo
mwenye magoli 39 akifuatiwa na Messi mwenye mabao 38.

0 comments:

Post a Comment