Facebook

Tuesday, 14 April 2015

Al Shabab yaua watu 9 Somalia.

Watu 9 wameripotiwa kuuawa katika majengo ya wizara ya elimu
mjini Mogadishu,Somalia.
Wavamizi hao walilipua bomu lililotegwa ndani ya gari kwenye ukuta wa jengo hilo
kabla ya wavamizi kadhaa kuingia ndani ya jengo wakiwa wamejihami
kwa bunduki za rashasha.

Msemaji wa wa kitengo cha mashambulizi cha kundi la wapiganaji wa
Al Shabaab Sheikh Abdiasis Abu Musab,
amethibitisha kuwa ni wao waliotekeleza shambulizi hilo na kuwa
''wapiganaji wetu wamekwisha ingia ndani ya jengo hilo lenye wizara
ya elimu''
Mapigano yanaendelea hadi sasa ndani ya jengo hilo baina ya
majeshi ya serikali na wapiganaji hao kulingana na mwakilishi wa
polisi.

Wapiganaji wa Al shabaab wametekeleza mashambulizi kama haya
katika siku za hivi punde.
Mwezi uliopita wapiganaji wa Al Shabaab walishambulia hoteli moja
mjini Mogadishu
Mwezi uliopita wapiganaji wa Al Shabaab walishambulia hoteli moja
mjini Mogadishu uvamizi huo ulikamilika siku mbili zilizofwatia .

Waandishi wa habari walioshuhudia matukio kabla ya uvamizi huo
wanadai kuwa kulikuwa na milipuko miwili mikubwa kabla ya milio ya
risasi kuanza kusikika kutoka jengo hilo.
hakuna kundi lililothibitisha kutekeleza shambulizi hilo lakini Al
shabaan imekuwa ikitumia mbinu kama zilizotumika leo.

Kundi hilo la waislamu linapinga serikali iliyoko sasa ambayo inaungwa
mkono na majeshi ya Umoja wa Afrika.

Related Posts:

  • Mchakato wa katiba kusitishwaKumekuwa na maoni tofauti kufuatia hatua ya kusitisha mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya nchini Tanzania. Katika kikao cha Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete na Viongozi wa vyama vya siasa nchini humo wamekubaliana kuwa ku… Read More
  • Binti alazimisha penzi kwa kumshikia Bastola mwanaume.Marekani: Binti (25) akamatwa kwa kosa la kumlazimisha kijana (33) kufanya naye mapenzi akiwa kamshikia bastoka kwenye gari lake baada ya kijana huyo kuomba lift. Inasemekana huyo binti alikuwa na mwanamke mwingine ambaye wal… Read More
  • Miaka 8 jela kwa jaribio la kutaka kumuua mkosoaji wa Rais wa RwandaWatu wanne - Watanzania wawili na Wanyarwanda wawili- waliokutwa na hatia ya kutaka kumuua mkosoaji wa Rais wa Rwanda Paul Kagame nchini Afrika Kusini wamehukumiwa kwenda jela kwa miaka minane kila mmoja. Mkuu wa zamani wa je… Read More
  • Nyama ya Kiboko yawaletea maafa Afrika KusiniWatu kumi walikanyagwa na gari lililokuwa linakwenda kwa mwendo wa kasi walipokuwa wanajaribu kujipatia angalau kipande cha nyama ya Kiboko mwishoni mwa wiki. Taarifa hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation. Kiboko huyo … Read More
  • Mahakama:Pistorius hakukusudia kuuaJaji anayetoa uamuzi katika kesi ya mauaji inayomkabili Oscar Pistorius, amesema upande wa mashitaka umekosa kuthibitishia kikamilifu shitaka kuu la kwanza dhidi ya Pistorius kuwa alikusudia kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp… Read More

0 comments:

Post a Comment