Facebook

Friday, 10 April 2015

IBRAHIMOVIC AFUNGIWA MECHI NNE

Mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic
amefungiwa kucheza mechi nne za ligi kuu ya Ufaransa baada ya
kunaswa na picha za televisheni akitukana.
Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Sweden alikasirika na
kuwashutumu waamuzi na pia kutukana baada ya timu yake kupoteza
3-2 dhidi ya Bordeaux mwezi uliopita. Ibrahimovic, 33, baadaye
aliomba radhi na kusema matamshi yake

"hayakuwa yamelenga
Ufaransa au wananchi wake".
Atakosa mechi nne kati ya saba zilizosalia za ligi. Kamati ya nidhamu
ilisema adhabu hiyo imezingatia "aina ya kosa na uzito wa matamshi
yake".

Ibrahimovic pia atakosa mchezo wa kwanza wa robo fainali ya
Champions League dhidi ya Barcelona kufuatia kadi nyekundu
aliyopewa katika mchezo uliopita dhidi ya Chelsea. Hata hivyo
ataweza kucheza mechi ya fainali ya kombe la ligi siku ya Jumamosi
dhidi ya Bastia.

Related Posts:

  • Tetesi zote za Usajili wa wachezaji barani Ulaya siku ya leo.Dau la Manchester United la pauni milioni 110 kwa Real Madrid kumtaka Gareth Bale, 25 na beki Rafael Varane, 22 limekataliwa na klabu hiyo ya La Liga (Daily Express),   Real Madrid wana uhakika wa kumsajili kwa pauni m… Read More
  • Uzinduzi wa jezi mpya Tifa Stars kuambata na tuzo maalumu. SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), kesho Jumatano linatarajia kuzindua jezi mpya za timu za Taifa Tanzania, zitakazokuwa zikitumika katika michuano mbalimbali, uzinduzi huo utakafanyika katika hoteli ya JB Belmonte (PS… Read More
  • Jack Wilshare ashtakiwa na FA. Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere ameshtakiwa na chama cha soka cha England, FA kufuatia tukio la kwenye msafara wa basi wakati wa kusherekea ushindi wa Kombe la FA. Taarifa ya FA imesema: "Inatuhumiwa kuwa tabia yake ya k… Read More
  • Berbatov afungashiwa virago Monaco. MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa waBulgaria, Dimitar Berbatov anatafuta timu ya tatu ya kujiunganayo England, baada yakutemwa na AS Monacoya Ufaransa. Berbatov alijiunga na vigogo hao wa Ligue 1 Januari mwaka 2014 ku… Read More
  • Maneno ya Blatter baada ya kujiuzulu. “Nilijiskia mkamilifu kwa kugombea tena kwenye uchaguzi wa FIFA nikiamini kwamba kilikua ni kitu muhimu kwa FIFA. Uchaguzi umeisha lakini changamoto za FIFA hazijaisha. Japokua nina madaraka kutoka kutoka kwa wanachaman… Read More

0 comments:

Post a Comment