Facebook

Saturday 4 April 2015

Uchambuzi Mechi zote kali Ligi Kuu Uingereza leo Jumamosi.

Baada ya mapumziko ya siku kadhaa kupisha mechi za kirafiki za timu za Taifa pamoja na michezo ya kugombea kucheza kombe la mataifa Ulaya litakalo fanyika Ufaransa mwakani ligi mbalimbali zina endelea wikiendi hii.
  
      ARSENAL vs LIVERPOOL
                  14:45
     MAN UTD vs A.VILLA
                  17:00
      CHELSEA vs STOKE
                  19:30

    Tukianzia ktk dimba la Emirates Arsenal walio nafasi ya 3 kwa pointi 60 watacheza dhidi ya Liver walio nafasi ya 5 kwa pointi 54.
     Kuelekea ktk mchezo huo Arsenal wameshinda michezo 5 huku Liver wakishida michezo 4 na kupoteza 1 mbele ya Utd kwa mara ya kwanza tangu mwaka huu uanze.
      Arsenal wapo ktk kiwango bora hivi sasa wakiongozwa na Giroud mchezaji bora wa mwezi uliopita pamoja na Wenger akiwa kocha bora wa mwezi mara ya mwisho kupoteza ktk ligi ilikuwa mbele ya Spurs (2-1) mwezi wa pili tangu hapo wamekuwa na matokeo mazuri michezo 10 wamepoteza mara 1.
     Liverpool sio wabaya kwani kabla ya kupoteza dhidi ya Man Utd walikuwa hawajapoteza, kiwango dhohofu kilipelekea kupoteza mchezo huo wataingia kwenye mchezo huu kwa presha ya kuendelea kusaka nafasi 4 za juu huku bado wakiendelea tafakari kauli tata ya Sterling.
    Mchezo uliopita kati ya timu hizi tulishuhudia sare ya (2-2) lakini kwa upande mwingine hawajawa na matokeo mazuri  pale Emirates kwani wameshinda mara 1 kati ya 18 ktk michuano mbalimbali ( W1,D7,L10) pia ni mchezo mmoja tu ambao hawajaruhusu goli mbele ya Arsenal pale Emirates hivyo kutokana na takwimu hizi na hali ya msimamo ilivyo mchezo utakuwa mgumu sana upande wao.
    Huu ndo mchezo wenye hatrick nyingi ktk ligi (5)  asilimia kubwa Arsenal wana nafasi ya kushinda kulingana na kuimalika kila siku huku chagizo likiwa ni kupata pointi 3 na kukwea hadi nafasi ya 2 ya msimamo wa ligi (63 pointi, City 61).

    Licha ya Arteta,Debuchy,Diaby na Wilshere kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Brentford bado watakuwa na nafasi ndogo kuanza dhidi ya Liver hivyo tutaraji kikosi kilekile kilicho cheza michezo ya hivi karibuni ingawa kwa Welbeck haija julikana kutokana na maumivu aliyo yapata kwenye mchezo dhidi ya Lithuania ktk timu yake ya taifa, upande wa Liver watamkosa Skirtel na Gerrard.

---------

    Ni wachache sana walio ipa Utd nafasi ya kufika hapa walipo pointi 59 nafasi ya 4 na wakishinda mchezo huu watakwea hadi nafasi ya 2 kwa pointi 62 na itakuwa kwa mara ya kwanza ktk kipindi kirefu.
   Ushindi mbele ya Liver ambayo ilikuwa na matokeo mazuri mwaka huu inaweza kuwa ni chachu ya kikosi cha Van Gaal kufanya vyema mbele Villa iliyo nafasi ya 16-28 chini ya Tim Sherwood.
   Tutaraji kukiona kikosi kilekile kilicho cheza dhidi ya Liver huku kikichagizwa na kiwango bora cha Mata na safu ya kiungo.
    Villa watamkosa Cleverley kwani ni mchezaji alie kwa mkopo toka Utd, zaidi ya hapo kikosi chote kilicho cheza mechi za hivi karibuni kipo fiti.
     Hawana matokeo mazuri mbele ya Man Utd mchezo wa awamu ya kwanza ulio kuwa na kasi sana pale Villa Park ilikuwa sare ya 1-1 ( Benteke,Falcao) kwenye michezo 11 wameshindwa kupata pointi tatu huku ushindi wao wa mwisho ukiwa ni 2009 kwa goli la Agbonlahor.
   Villa wata ingia kwa mashambulizi ya kustukiza huku macho yao yakiwa kwa ( Sinclair,Benteke,Agbonlahor) ambao watakuwa mwiba mbele ya safu ya Utd.
   Licha ya kutokuonyesha kiwango mchezo dhidi ya Liver Rooney amekuwa na takwimu nzuri mbele ya Villa amefunga mara nyingi (12).

-------

   Wakiwa nafasi ya 10 kwa pointi 42 huku akichagizwa na matumaini ya mkataba mpya (3yrs) Mark Hughes atakuwa London kucheza dhidi ya wenyeji wake Chelsea walio kileleni kwa pointi 67 na mchezo 1 wa kiporo.
    Stoke watamkosa Moses kwani ni mchezaji wa Chelsea alie kwa mkopo hivyo tegemezi litakuwa hasa kwa Crouch anaetafuta rekodi ya wingi wa mabao ya kichwa kumfikia ( Alan Shearer-46) .
   Chelsea wameshinda mara 10 kati ya 13 dhidi ya Stoke wakipoteza mchezo 1,hawajaruhusu goli michezo 6 kati ya 7 dhidi ya Stoke.

For more/ Ushauri::
Choikangta.ckt@gmail.com

0 comments:

Post a Comment