Facebook

Tuesday 28 April 2015

Babake mzazi Kim Kardashian ajitangaza kuwa ni 'Mwanamke'

Bruce Jenner aliyekuwa mwariadha bora duaniani kabla ya kuwa
nyota wa kipindi cha televisheni na familia moja maarufu duniani
''The Kardashians''. sasa amefichua siri ambayo amekuwa akiificha
kwa miaka mingi.
''Kwa nia na madhumuni yote, mimi ni mwanamke.'' Jenner aliambia
Sawyer kutoka ABC katika mahojiano maalum yaliopeperushwa hewani
siku ya Ijumaa.
''Watu wananiona tofauti,wananiona kama mwanaume, lakini moyo na
roho yangu na kila kitu ninachofanya maishani ni sehemu yangu.''
Jenner ambaye ana umri wa miaka 65 amesema. '' Upande huu wa
kike ni sehemu yangu.
hivi ndivyo mimi nilivyo.''
Bruce Jenner
Katika masaa ya mahojiano na Diane Sawyer mjini New York na
California, Jenner alielezea kwa kina mapambano yake ya kuwa na
jinsia mbili tangu utotoni.
''Akili zangu ni za kike sana kuliko za kiume.'' Ameongezea. '' Ni
vigumu sana watu kuelewa, lakini hivyo ndivyo nafsi yangu ilivyo.''
Jenner aliyejawa na hisia na mwenye nywele ndefu shati na suruali
ndefu alisema kuwa amesubiri kwa miaka mingi ili kujitangaza kwa
kuwa hakutaka kuwavunja moyo watu.
Kwa miongo kadhaa wake wa zamani wa Jenner na madada zake
waliweka siri kuhusu jinsia yake na kwamba walikuwa watu waliokuwa
wakijua siri hiyo.
Mtandao wa watu wanaojua siri hiyo hatahivyo ulipanuka hivi majuzi
wakati Jenner alipomwambia mamaake na wanawe 10 .
Jenner ana watoto sita Burt,Cassandra,Brabdon,Brody,Kendall na
Kylie pamoja na watoto wanne wa kambo akiwemo Kourtney,Kim,Khloe
na Rob Kardashian.

0 comments:

Post a Comment