Bruce Jenner aliyekuwa mwariadha bora duaniani kabla ya kuwa
nyota wa kipindi cha televisheni na familia moja maarufu duniani
''The Kardashians''. sasa amefichua siri ambayo amekuwa akiificha
kwa miaka mingi.
''Kwa nia na madhumuni yote, mimi ni mwanamke.'' Jenner aliambia
Sawyer kutoka ABC katika mahojiano maalum yaliopeperushwa hewani
siku ya Ijumaa.
''Watu wananiona tofauti,wananiona kama mwanaume, lakini moyo na
roho yangu na kila kitu ninachofanya maishani ni sehemu yangu.''
Jenner ambaye ana umri wa miaka 65 amesema. '' Upande huu wa
kike ni sehemu yangu.
hivi ndivyo mimi nilivyo.''
Bruce Jenner
Katika masaa ya mahojiano na Diane Sawyer mjini New York na
California, Jenner alielezea kwa kina mapambano yake ya kuwa na
jinsia mbili tangu utotoni.
''Akili zangu ni za kike sana kuliko za kiume.'' Ameongezea. '' Ni
vigumu sana watu kuelewa, lakini hivyo ndivyo nafsi yangu ilivyo.''
Jenner aliyejawa na hisia na mwenye nywele ndefu shati na suruali
ndefu alisema kuwa amesubiri kwa miaka mingi ili kujitangaza kwa
kuwa hakutaka kuwavunja moyo watu.
Kwa miongo kadhaa wake wa zamani wa Jenner na madada zake
waliweka siri kuhusu jinsia yake na kwamba walikuwa watu waliokuwa
wakijua siri hiyo.
Mtandao wa watu wanaojua siri hiyo hatahivyo ulipanuka hivi majuzi
wakati Jenner alipomwambia mamaake na wanawe 10 .
Jenner ana watoto sita Burt,Cassandra,Brabdon,Brody,Kendall na
Kylie pamoja na watoto wanne wa kambo akiwemo Kourtney,Kim,Khloe
na Rob Kardashian.
Tuesday, 28 April 2015
Babake mzazi Kim Kardashian ajitangaza kuwa ni 'Mwanamke'
Related Posts:
Mtanangazaji maarufu CNN "abwaga manyanga"Mtangazaji wa TV Piers Morgan ameacha kazi katika shirika la habari la Marekani la CNN, licha ya kupewa nafasi ya kuongeza mkataba wake. Morgan ame tweet akisema anakwenda "kujaribu mambo mengine mapya" baada ya wakuu wa … Read More
Diamond awaomba mashabiki kumpigia kura Tuzo za Channel O Ni hatua kubwa anazozidi kuzipiga msanii wa kizazi kipya nchini,Diamond Platnumz,ambaye hivi sasa anaipeperusha vyema bendera ya Taifa hili. Ni katika hatua nyingine ambayo mafanikio yanazidi kusogea,Diamond kup… Read More
Mchekeshaji maarufu aaga duniaMchekeshaji maarufu nchini Marekani Joan Rivers amefariki dunia akiwa na umri wa miaka themanini na na mmoja. Joan alikuwa amelazwa katika hospitali moja mjini New York kwa wiki kadhaa sasa akisumbuliwa na maradhi ya moyo. Me… Read More
"GETO" LA BALOTELLI?Mario Balotelli ndio kwanza amerejea England, kwa mara ya pili, lakini inaonekana haijamchukua muda mrefu kugonga vichwa vya habari, safari hii kwa kuonesha "ladha" ya mitindo na mambo anayopenda. Mchezaji huyo wa Liverpool a… Read More
JUSTIN BEIBER ASHITAKIWA KWA UENDESHAJI MBAYA WA GARI Ni jumanne nyingine,huku skendo nyingine ya Justin Beiber ikigonga vichwa vya watu mbalimbali. Polisi wa Canada wanasema Justin ameshitakiwa kwa kuendesha gari vibaya pia kutoa lugha chafu. Hii inafuatia baada ya gari lake … Read More
0 comments:
Post a Comment