Facebook

Tuesday 28 April 2015

Watu zaidi ya 5000 wafariki dunia baada ya tetemeko kubwa la ardhi huko Nepal.

Idadi ya watu ambao wamethibitishwa kuaga dunia wakati
kulipotokea tetemeko kubwa la ardhi nchini Nepal siku ya Jumamosi
imepanda hadi zaidi ya watu 5000.
Utawala unasema kuwa zaidi ya watu 10,000 walijeruhiwa. Serikali ya
Nepal inasema kuwa imelemewa na kiwango cha janga hilo.
Waziri mkuu Sushil Koirala anasema kuwa utawala unapokea maombi
mengi ya kutaka msaada kutoka maeneo ya mbali ya vijiji vya
Himalaya, lakini jitihada za kuyafikia maeneo hayo zinatatizwa na
uhaba wa vifaa na waokoaji.
Waziri huyo mkuu anasema kuwa kuna mahitaji ya dharura ya
mahema , chakula na maji.Zaidi ya nusu ya nyumba katika kijiji hicho zimeharibiwa.

0 comments:

Post a Comment