Facebook

Wednesday 8 April 2015

IFAHAMU HISTORIA YA KLABU YA ARSENAL FC.

Mwanzo hadi Vita ya Kwanza ya Dunia
Maisha ya klabu ya soka ya Arsenal yalianza pale
kikundi cha wafanyakazi katika kiwanda cha
kuzalisha zana za kivita cha Woolwich
walipoamua kuunda klabu ya soka mwishoni
mwa mwaka 1886. Klabu ikawa ikishiriki michezo
huku ikijulikana kama Dial Square. Mchezo wao
wa kwanza waliifunga timu ya Eastern Wanderers
6-0, tarehe 11 Desemba 1886.

Baada ya muda mfupi, jina likabadilishwa na kuwa
Royal Arsenal huku timu ikiendelea kushiriki katika
michezo ya kirafiki na mashindano ya nyumbani kwa
kipindi cha miaka michache iliyofuata.

Mwaka 1891 klabu ikawa ya kulipwa na kubadilisha
jina na kuitwa Woolwich Arsenal na hatimaye
kujiunga na ligi ya soka mwaka 1893. ‘Washika
bunduki’ hao wakahamia Highbury mwaka 1913 kama
timu ya ligi daraja la pili. Baada ya Vita ya Kwanza ya
Dunia, Arsenal wakapigiwa kura na kuingizwa katika
ligi daraja la kwanza, iliyokuwa imeongezwa ukubwa,
ambako wameendelea kudumu hadi leo.
Chapman na kipindi cha mafanikio miaka ya 1930

Itaendelea

Imeandaliwa na Emmanuel Noel.

0 comments:

Post a Comment