Facebook

Wednesday, 8 April 2015

IFAHAMU HISTORIA YA KLABU YA ARSENAL FC.

Mwanzo hadi Vita ya Kwanza ya Dunia
Maisha ya klabu ya soka ya Arsenal yalianza pale
kikundi cha wafanyakazi katika kiwanda cha
kuzalisha zana za kivita cha Woolwich
walipoamua kuunda klabu ya soka mwishoni
mwa mwaka 1886. Klabu ikawa ikishiriki michezo
huku ikijulikana kama Dial Square. Mchezo wao
wa kwanza waliifunga timu ya Eastern Wanderers
6-0, tarehe 11 Desemba 1886.

Baada ya muda mfupi, jina likabadilishwa na kuwa
Royal Arsenal huku timu ikiendelea kushiriki katika
michezo ya kirafiki na mashindano ya nyumbani kwa
kipindi cha miaka michache iliyofuata.

Mwaka 1891 klabu ikawa ya kulipwa na kubadilisha
jina na kuitwa Woolwich Arsenal na hatimaye
kujiunga na ligi ya soka mwaka 1893. ‘Washika
bunduki’ hao wakahamia Highbury mwaka 1913 kama
timu ya ligi daraja la pili. Baada ya Vita ya Kwanza ya
Dunia, Arsenal wakapigiwa kura na kuingizwa katika
ligi daraja la kwanza, iliyokuwa imeongezwa ukubwa,
ambako wameendelea kudumu hadi leo.
Chapman na kipindi cha mafanikio miaka ya 1930

Itaendelea

Imeandaliwa na Emmanuel Noel.

Related Posts:

  • MAYWEATHER KUZICHAPA TENA NA MAIDANA Floyd Mayweather ametangaza kuwa atapanda ulingoni kupambana na Marcos Maidana, Septemba 3 mwaka huu mjini Las Vegas. Mayweather alimzidi Maidana katika mpambano uliozua utata mwezi Mei, na alisema kuwa atarudiana na … Read More
  • David Rudisha azidi kung'ara Olimpiki.   David Rudisha ameshinda mbio za mita 800 wanaume katika mbio za Diamond League za Scotland. Mara ya mwisho kuwa nchini Uingereza Rudisha alishinda medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki ya London 2012. Mwa… Read More
  • Refa wa fainali za Kombe la Dunia atajwa....!              Nicola Rizzoli amechaguliwa na Fifa kuwa mwamuzi katika mchezo wa fainali - Kombe la Dunia Brazil 2014 kati ya Ujerumani na Argentina.  &n… Read More
  • FIFA YATANGAZA WATAKAOWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA Fifa imetangaza orodha ya majina 10 watakaowania tuzo ya mchezaji bora katika michuano ya Kombe la Dunia - 2014 Golden Ball. Wachezaji watatu wametoka Argentina, Angel Di Maria, Javier Mascherano na Lionel Messi. Maha… Read More
  • LIVERPOOL NA BARCA WAKUBALIANA JUU YA SUAREZ   Liverpool wamefikia makubaliano ya kumuuza Luis Suarez kwenda Barcelona. Ada ya uhamisho inadhaniwa kuwa takriban pauni milioni 75. Suarez alijiunga na Liverpool mwaka 2011 akitokea Ajax, kwa pauni milioni 22.7. A… Read More

0 comments:

Post a Comment