Facebook

Sunday 27 April 2014

Atletico Madrid yashinda,yaukaribia ubingwa..............

Photo: Play like every match is your last. Atlético de Madrid
WAKICHEZA Ugenini huko Estadio de Mestalla, Vinara wa La Liga, Atletico Madrid wameifunga 

Valencia goli 1-0 na kupaa kileleni wakiwa Pointi 6 mbele ya Timu ya Pili, Real Madrid.
Atletico,ambaoJumatano wanasafiri kwenda Stamford Bridge kurudiana na Chelsea kwenye Nusu Fainali ya UEFA , wanahitaji Pointi 6 tu katika Mechi zao 3 zilizobaki ili wawe Mabingwa.
Bao la Atletico lilifungwa na Raul Garcia katika Dakika ya 43 kwa Kichwa alipounganisha Krosi ya Gabi.
Atletico walimaliza Mechi hii wakiwa Mtu 10 wakati Mchezaji wao Juanfran alipopewa Kadi Nyekundu kwa Rafu mbaya katika Dakika za Majeruhi.

VIKOSI:
VALENCIA: Guaita; J.Pereira, R.Costa, Mathieu; Gaya; Fuego, Parejo; Barragan, Jonas, Piatti; Alcacer.
ATLETICO: Courtois; Juanfran, Miranda, Godin, Filipe Luis; Tiago, Gabi, Koke, Raul Garcia; David Villa, Diego Costa.
 

MSIMAMO-Timu za Juu:
NA TIMU P W D L F A GD PTS
1 Atletico de Madrid 35 28 4 3 75 22 53 88
2 Real Madrid CF 34 26 4 4 98 32 66 82
3 FC Barcelona 34 26 3 5 94 28 66 81
4 Athletic de Bilbao 34 18 8 8 59 37 22 62

0 comments:

Post a Comment