Facebook

Sunday 27 April 2014

Mbio za Ubingwa zaanza upya ....Liverpool yachapwa..Mourinho anafanya anachowaza............


 

Chelsea wamewapa pigo kubwa Liverpool na ndoto yao ya kutwaa Ubingwa wao wa kwanza katika Miaka 24 na wao kujiwekea matumaini baada ya kushinda Bao 2-0 Uwanjani Anfield wakiwa wamechezesha ‘Kikosi hafifu’ huku jicho lao likiwa kwenye Mechi yao ya Marudiano ya Nusu Fainali ya Ligi ya mabingwa Ulaya Jumatano Uwanjani Stamford Bridge.
Mashabiki wa Liverpool walikusanyika kwa ajili ya Mechi hii wakiwa na hakika ya ushindi, hasa baada Jose Mourinho kudokeza atachezesha ‘Kikosi hafifu’, na kabla ya Mechi kuanza Basi lililobeba Wachezaji wa Liverpool lilipokuwa kwa shangwe kubwa nje ya Anfield mithili ya Paredi ya Ubingwa.
Pengine huu ndio Msemo wa kule kwetu Mwaneromango: “WACHEKELEA MBELEKO, MWANA BADO!”
Bao zilizoiua Liverpool zilifungwa na Demba Ba katika Dakika ya 45 baada ya Nahodha Steven Gerrard kuteleza na Demba Ba kunufaika na kwenda kufunga na la Pili kupigwa Dakika za Majeruhi na Willian, alietokea Benchi, alipopokea Pasi murua ya Fernando Torres.

Ushindi huu umewaacha Chelsea wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Liverpool lakini huenda matokeo haya yakawanufaisha sana Manchester City ambao wana Mechi mbili mkononi na wakishinda zote wataikamata Liverpool na kuongoza kwa Ubora wao wa Magoli.

 MATUKIO MBALIMBALI KWENYE MECHI HIYO

Photo: The Fighting SpiritPhoto: We have turned Anfield Blue :)Photo: Ba's goal :)
Photo 

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata habari za michezo pamoja na picha za mchezo huo kwa wakati muafaka bila zengwe

0 comments:

Post a Comment