Facebook

Sunday 27 April 2014

Simba wachukua maamuzi magumu,watema kikosi kizima............

 

UKITAKA mafanikio lazima uchukue uamuzi mgumu ambao hakuna anayeweza kufikiria kabla.

Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic amesema analazimika kutema wachezaji wasiopungua 11 ambao ni sawa na kikosi kizima kinachoweza kucheza mechi ya ushindani.


Lengo la Logarusic kufanya hivyo ni ili aweze kujenga upya timu ya ushindani msimu ujao.


Logarusic sasa ana uhakika wa kubaki Simba, baada ya kuhakikishiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Pope kwani awali hakuwa na uhakika wa kuendelea kubaki katika timu hiyo kutokana na mkataba wake kumalizika.


Kocha huyo atasaini mkataba wa miaka miwili baada ya ule wa miezi sita kufikia tamati.


Katika ripoti yake kwa uongozi wa timu hiyo, Logarusic amewaeleza wazi viongozi wake kuwa, ili Simba iwe na ushiriki mzuri msimu ujao wa Ligi Kuu Bara lazima nyota 11 wa timu hiyo waachwe ili wapatikane wengine watakaoisaidia timu kufikia mafanikio.

0 comments:

Post a Comment