Facebook

Wednesday 30 April 2014

Uchambuzi: Bayern Munich 0-4 Real Madrid


 
Ushindi wa Madrid wa bao 4-0 magoli mawili kila mmoja kwa Sergio Ramos na Cristiano Ronaldo yameivusha Madrid kwenda katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Mei 24 pale Lisbon Ureno kwa ushindi wa Jumla wa magoli 5-0.
KWA MATOKEO HAYO:-
> Real Madrid imefika fainali yake ya 13 tangu ianze kushiriki michuano hiyo huku ikiwa imeshachukua kombe hilo mara 9.
> Real Madrid licha ya kuwa timu yenye mafanikio na historia kubwa katika michuano hiyo wamesota miaka 12 mpaka kupata nafasi ya kucheza fainali mwaka huu mara ya mwisho ilikua mwaka 2002.
> Real Madrid ndo timu ya kwanza kuifunga Bayern 4-0 nyumbani kwao Alianz Arena katika mashindano yote mara ya mwisho kufungwa 4-0 nyumbani ilikua mwaka 1979
> Ronaldo amefunga goli lake la 16 msimu huu na kuvunja kabisa rekodi zote zilizowekwa awali na  Jose "Mazzola" Altafini wa AC Milan mwaka 1962/1963 na Lionel Messi mwaka 2011/2012.
>  kutolewa kwa Bayern Munich ambao wengi tuliamini angetetea taji hilo imepelekea Historia kuzidi kuendelezwa kwa bingwa mtetezi kushindwa kutetea taji lake katika michuano hiyo.
MIWANI PANA YA KATEMI:-
Mimi Katemi naamini Anachokifanya Pep Guadiola (Kocha wa Bayern) kuibadilisha Timu hiyo kiuchezaji imefanikiwa mno na bado kitambo kidogo Bayern itakua moto wa kuotea mbali ila atafanikiwa kama atapata mabeki wenye kasi na wanaoweza kupanda na kurudi kulinda lango hapa nawaona Laurent Koscienly wa Arsenal, Vicent Kompany wa Man City au David Luiz wa Chelsea kama wachezaji sahihi wa kuchukua nafasi ya Dante na Boateng katika safu ya ulinzi.
Real Madrid ina kila sababu ya kubeba ubingwa mwaka huu kwani ndo timu iliyokamilika kila idara kwa  miwani yangu paaaaaaana na kwahilo mpira tutakua tumeutendea haki.

0 comments:

Post a Comment