Wednesday, 23 April 2014
Paul Makonda awaita UKAWA watoto wa shetani na kagoma kufuta kauli.....................soma hapa..............................
Mjumbe wa Bunge la Katiba, Paul Makonda, jana aligoma kufuta kauli yake baada ya kuwaita viongozi wakuu wawili wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwa ni watoto wa shetani.
Akichangia bungeni, Makonda alisema Mwenyekiti wa Ukawa, Freeman Mbowe, Mwenyekiti mwenza , Profesa Ibrahim Lipumba na mjumbe wa Ukawa, Ismail Jussa ni watoto wa shetani.
Shetani alikuja duniani kuiharibu dunia na kuteketeza kila kilichostahili kuungana… Lakini Yesu alikuja kuponya na kurekebisha kile kilichopotea,” alisema na kuongeza:
“Bahati mbaya sana shetani ni baba wa uongo, watoto wake ni mheshimiwa Jussa, watoto wake ni mheshimiwa Mbowe, watoto wake ni mheshimiwa Lipumba…Hawa ni watoto wa shetani.” Makonda aliwataka vijana nchi nzima wasikubali kupoteza muda wake kuambatana na viongozi hao katika matembezi yao, badala yake wajikite katika kufanya kazi za kiuchumi na kujiingizia kipato. Hata hivyo, baada ya kauli hiyo, mjumbe mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, aliomba mwongozo wa Mwenyekiti akisema Makonda alikuwa ametumia lugha ya kuudhi na isiyofaa.
“Huwezi kumwita mwanadamu mwenzako shetani… Aombe radhi na aondoe kauli hiyo mara moja” alisema na kumlaumu Mwenyekiti, Samuel Sitta kwa kuruhusu hali hiyo.
Sitta alisema “Ni kweli haipendezi kuitwa shetani nitamuomba mheshimiwa Paul Makonda aliangalie katika mazingira yetu na aweze kuyafuta hayo maneno”.
Hata hivyo, Makonda alisisitiza kuwa hawezi kufuta kauli yake wala kuomba radhi kwa sababu alikuwa amenukuu Biblia inayosema shetani ni baba wa uongo.
Baada ya kauli hiyo, Sitta alimtaka mjumbe aliyeomba mwongozo kurudi kwenye kanuni ili suala hilo liweze kupelekwa kamati ya maadili kama atataka kufanya hivyo.
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata taarifa mbalimbali kuhusu mchakato wa katiba mpya
Related Posts:
Muangalie hapa Waziri wa Nishati na Madini,Prof.Muhongo akiombewa kabla ya kwenda kuwasilisha ripoti.Prof Muhongo akiombewa leo asubuhi na wachungaji pamoja na mashekhe!! Kabla ya kwenda kuwasilisha ripoti ya Wizara ya Nishati na madini inayosadikika kukumbwa na wimbi la ufisadi. … Read More
BantuTz MAGAZINE-Soma kilichoandikwa katika Magazeti ya leo Novemba 28. BantuTz MAGAZETI:Ni miongoni mwa huduma bora kabisa tunazozitoa ili wewe mdau wa Bantu usipitwe na habari,stori au taarifa yoyote ile.Tunakuletea kila tunachokipata kwa wakati na muda muafaka.Soma kilichoandikwa kati… Read More
LIVE !! BUNGENI DODOMA-SAKATA LA AKAUNTI YA ESCROW. Habari wakuu, Baada ya jana ripoti kusomwa, Kama kawaida moja kwa moja kutoka bungeni Dodoma tutajuzana hapa kupitia BantuTz.com. Kwa wale wasio na uwezo kufatilia moja kwa moja pia kwa wale wenye nafasi ya kufatili… Read More
Zitto kufanya majumuisho ya kamati ya PAC leo hii jioni na kujibu hoja inayomkabili. Hiki ndicho alichoandika kupitia ukurasa wake wa facebook Leo jioni kuanzia saa Kumi na Moja nitafanya majumuisho ya hoja ya Kamati ya PAC kuhusu akaunti ya Escrow na uhalali wa Kampuni ya PAP kumiliki IPTL. … Read More
ASKOFU KILAINI AKIRI KUPOKEA MILIONI 80.5. Askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba Methodius Kilaini amekiri kupokea milioni 80.5 kutoka kwa James Rugemalira na akisema hii si mara yake ya kwanza kupokea fedha toka kwa mfanyabiashara huyo kwakuwa mara nyingi hu… Read More
0 comments:
Post a Comment