Facebook

Friday, 18 April 2014

Barca Majanga....Alba na Neymar Nje wiki nne.......soma hapa....

388904_heroa
 Mshambuliaji wao raia wa Brazil, Neymar ataa nje ya uwanja wa wiki nne, wakati naye beki Jordi Alba atakaa muda kama huo baada ya wote kupata majeruhi.
Klabu ya Barcelona imethibitisha kuwa Neymar alipata majeruhi ya mguu jana katika mchezo wa fainali ya kombe la Mfalme dhidi ya Real Madrid.
Kinda huyo mwenye miaka 21 alishindwa kuisaidia Barca kuepukana na kipigo cha mabao 2-1, huku Mbrazil huyo akikosa nafasi ya wazi dakika za lala salama.
Neymar atakosa mechi zijazo dhidi ya Athletic Bilbao, Villarreal, Getafe na Elche.
Hata hivyo klabu ya Barca ina matumaini kuwa nyota wake huyo anaweza kurudi katika mechi ya mwisho dhidi ya Atletico Madrid.
Taarifa ya klabu ya Barcelona imesema;”Mchezaji huyu aliumia jana katika mguu wake wa kushoto na anahitaji muda maalumu wa matibabu. Makadirio ya kurudi uwanjani ni wiki nne”.
Naye Jordi Alba alitolewa baada ya dakika 45 za kipindi cha kwanza katika mechi ya jana na taarifa zinaeleza kuwa beki huyo wa kushoto aliumia nyama za paja za mguu wake wa kulia.
Beki huyo wa zamani wa Valencia anaweza kukaa nje ya uwanja kwa wiki tatu hadi nne

Related Posts:

  • NINACHOAMINI MAESTRO:-GEGENPRESSING KUTOKA KWA SUPER JURGEN KLOPP. Na: Ayoub Hinjo(Ayo's Mata Maestro) Mafanikio yoyote huja baada ya kuwa na mipango thabiti ndani yake,kamwe huwezi kuwa kwenye mafanikio kama hutakuwa na mipango iliyonyooka na yenye msimamo ndani yake. Uthabiti wa mipango ya… Read More
  • Suleiman Matola aachia ngazi Simba SC.Kocha msaidizi wa simba Suleiman Abdallah Matola amejiuzulu nafasi hiyo kutokana na kile alichodai kutolelewana na Kocha Mkuu, Muingereza, Dylan Kerr. Matola amesema kwamba amefikia uamuzi huo baada ya kuona maelewano na bosi… Read More
  • Matola aachia ngazi Simba SC.Kocha msaidizi wa simba Suleiman Abdallah Matola amejiuzulu nafasi hiyo kutokana na kile alichodai kutolelewana na Kocha Mkuu, Muingereza, Dylan Kerr. Matola amesema kwamba amefikia uamuzi huo baada ya kuona maelewano na bosi… Read More
  • Sepp Blatter alazwa baada ya mshutuko. Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa, Sepp Blatter amelazwa hospitalini kutokana na kupatwa mshituko wa neva. Blatter aliyesimamishwa kwa siku 90 kujishughulisha na masuala ya soka wakati akichunguzwa kwa kashfa za rushwa … Read More
  • MEMPHIS DEPAY NA MIPANGO YA KURUDI KWENYE KIWANGODepay: "Khali Ni Ngumu Unapokuwa Benchi,Lakini Ni Nzuri Kwa Sasa Na Itakuwa Nzuri Mazoezini Pia. Kwahiyo Nikipata Nafasi Ya Kucheza.,Nitaitumia" Depay: "Mambo Mengi Yamebadilika.,Niko Kwenye Klabu Mpya Kwa Sasa, Na Ligi Ya Ki… Read More

0 comments:

Post a Comment