Wednesday, 23 April 2014
Waisalamu na Maaskofu waungana kutetea rasimu ya Warioba.......................fuatilia hapa............
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania imeungana na maaskofu mbalimbali kuwataka wajumbe wa Bunge la Katiba kuheshimu Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa kwa mujibu wa sheria na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Pia, taasisi hiyo imemtaka Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi kutokana na kauli waliyodai ya kichochezi, aliyoitoa katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma kuwa ukipitishwa muundo wa serikali tatu, jeshi litachukua nchi kwa sababu itashindwa kuwalipa mishahara.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Msemaji wa Jumuiya na Taasisi hizo, Sheikh Rajab Katimba alilaani kauli kuhusu jeshi na kuwa makanisa yote yatafungwa na nchi itakosa amani kutokana na kupitisha muundo huo wa serikali.
Sheikh Katimba alisema Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba imetokana na utafiti na uchambuzi wa maoni ya wananchi wa Tanzania Bara na Visiwani ili kuboresha Muungano kutatua kero zilizodumu kwa miaka 50 sasa.
Msimamo
Jumuiya hiyo iliweka wazi msimamo wake wa kutaka serikali tatu na kutaka maoni ya makundi mbalimbali ndani ya Bunge la Katiba kuheshimiwa.
Mjumbe wa Jumuiya hiyo, Sheikh Ramadhan Sanze pia alisema si ustaarabu kwa kundi moja kuhodhi mchakato kwa masilahi binafsi.
Alisema kukosoa maoni ya waasisi wa Taifa si dhambi kwa sababu wao hawakuwa Mungu kwamba hawakosei, badala yake alipendekeza watu waachwe wazungumze kwa utashi wa matakwa yao juu ya kile kilichowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
“Nchi hii haithamini mchango wa wataalamu, tumeona Tume ilivyofanya kazi nzuri, leo hii wanatukanwa hadharani, nawashangaa sana viongozi wa nchi hii,” alisema.
Sheikh Sanze alisema miiko na misingi waliyoiweka waasisi wa Taifa inavunjwa na viongozi wenyewe ambao leo wanasema waasisi wanatukanwa kwa kuwa wamependekeza serikali tatu badala ya mbili walizounda waasisi.
“Kulikuwa na utaratibu wa kubadilishana awamu za uongozi katika Serikali ya Muungano, awamu hii rais akitoka Tanzania Bara, ijayo atatoka Zanzibar; hii ndiyo misingi waliyoiweka waasisi, mbona leo haifuatwi? Huu ni unafiki...” alifafanua Sheikh Sanze.
Jumuiya hiyo imewataka wananchi wote kuendelea na mshikamano katika kutengeneza Katiba Mpya yenye maridhiano na itakayoondoa kero zilizodumu kwa zaidi ya miaka 50.
Related Posts:
Dr.John Magufuli:Ajenda ni maendeleo na si kuchagua vyama.Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amewataka Watanzania kuweka vyama vyao pembeni, badala yake kuweka mbele ajenda ya maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni katika jimbo la… Read More
Wanachama 600 na viongozi 15 wa UKAWA Jimbo la Vunjo wahamia CCM.Taarifa tuliyoipokea kutoka jimbo la Vunjo ambalo Mwenyekiti wa Chama Cha NCCR MAGEUZI anagombea ubunge. Lakini baada ya hapo jana Bantuz.com kuripoti taarifa kuhusiana na kutokea kwa mgawanyiko wa wana-UKAWA katika jimbo hil… Read More
Lowassa awaambia wananchi wa Muleba wamfungie magoli 3.Wananchi wa Jimbo la Muleba Kusini wakizungusha mikono wakiashiria kutaka mabadiliko walipokuwa kwenye Uwanja wa Fatuma, Muleba ulipofanyika mkutano wa kampeni za mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa, mkoani Ka… Read More
CHADEMA wapanga kumshtaki Dr.John Magufuli kwa matumizi ya M4CDar es Salaam. Chama cha Chadema, kimesema kinakusudia kumfungulia mashtaka Dk John Magufuli kwa madai ya kutumia nembo yake ya ‘M4C Movement For Change’ ikiwa na maana “Vuguvugu la Mabadiliko” na kuig… Read More
Wakenya 3 wauawa kwa Ujambazi Arusha.Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas Arusha amesema Majambazi wane, wakiwemo raia watatu wa Kenya wameuwa na polisi mkoani Arusha baada ya kuhusika kufanya matukio mbalimbali ya ujambazi wa kupora silaha pamoja na… Read More
0 comments:
Post a Comment