Facebook

Friday, 25 April 2014

Kocha mpya wa Muda Man Utd,Ryan Giggs kukutana na waandishi wa habri leo hii....................


RYAN_GIGGS-MENEJA 
































Arudisha desturi zote za Sir Alex Ferguson
LEO hii, Ryan Giggs atafanya Mkutano wake wa kwanza na Wanahabari tangu ateuliwe kuwa Meneja mpya wa Manchester United.
Giggs aliteuliwa Siku ya Jumanne mara baada ya David Moyes kufukuzwa na Mkutano huo wa Leo utafanyika Saa 6 Mchana, Saa za Bongo, huko Aon Training Complex, Jijini Manchester ambako ndio Kituo cha Mazoezi cha Man United.
Giggs, mwenye Miaka 40, atafanya Kikao hicho kwenye chumba kilekile alichokuwa akitumia Sir Alex Ferguson kwa Mkutano wake wa kila Wiki tofauti na David Moyes aliekuwa akitumia Ukumbi mwingine.
Pia, kama alivyokuwa Sir Alex Ferguson, Giggs ameurudisha Mkutano huo wa kila Wiki wa Waandishi wa Habari, unaofanyika kila Ijumaa, kufanyika Asubuhi kabla ya kuanza Mazoezi wakati Moyes alikuwa akiufanya baada ya Mazoezi.
Mechi ya Kwanza ambayo Giggs atasimamia kama Meneja, akisaidiwa na Nicky Butt, Paul Scholes na Phil Neville, ni Jumamosi Uwanja wa Old Trafford dhidi ya Norwich City kwenye Ligi Kuu England.
Tayari Giggs ameshawataka Wachezaji wake kurudia kucheza kama Manchester United kwa kuzishambulia na kuzibana Timu kama walivyokuwa wanafanya chini ya Sir Alex Ferguson.
Giggs ataisimamia Man United kwa Mechi zao 4 za Ligi zilizobaki Msimu huu.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment