Facebook

Friday, 25 April 2014

Ronaldo,Messi na Neymar tayari wameshaibiwa "kombe la dunia"......................


STICKER-CR7-MESSI-NEYMAR 
WAKUSANYAJI wa Stika huko Jijini Rio De Janeiro, Brazil walipatwa na mstuko baada ya Gari lillilobeba Maelfu ya Stika za Aina ya Panini kuibiwa zikiwemo zile za Mastaa wakubwa Cristiano Ronaldos, Lionel Messis na Neymar.
Stika 300,000 zilizokuwemo ndani ya Gari hilo zilikuwa zikisambazwa kwenye Maduka yanayouza Magazeti ili Wakusanyaji wazinunue.

Stika hizo zenye Picha mbalimbali za Mastaa watakaocheza Fainali za Kombe la Kombe la Dunia huko Brazil Mwezi Juni hukusanywa na Washabiki na kubandikwa kwenye Vitabu au Ukutani.
Stika hizi za Aina ya Panini zilianza kutumika kwenye Fainali za Kombe la Dunia la Mwaka 1970.

Hata hivyo, Kampuni ya Panini imewahakikishia Washabiki kuwa zipo Stika za kutosha kwa wao kukamilisha idadi ya Stika 640 ambazo ndio za Wachezaji wote wakiwemo wale Masta wakubwa kabisa Cristiano Ronaldos, Lionel Messis na Neymar.
Hivi sasa Stika hizo ni maarufu mno huko Nchini Brazil ambako ndiko Fainali za Kombe la Dunia zitachezwa kuanzia Juni 12 hadi Julai 13 Mwaka huu.

Umaarufu wa Stika hizi umakua sana kiasi ambacho Watu, Vijana kwa Wazee, huingia Mitandaoni na kubadilishana Stika ili kutimiza Idadi ya Stika 640 ambazo ndio hufanya Albamu moja.
Kampuni ya Panini imesema inatarajia kuuza Albamu Milioni 8 huko Brazil.

Hii si mara ya kwanza kwa Stika za Panini kuibiwa kwani Mwaka 2010 huko Afrika Kusini, kabla kuanza kwa Fainali za Kombe la Dunia, Wezi walivamia Kituo cha Ugawaji wa Stika na kuzoa Paketi 135,000 lakini baadae zilikamatwa.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment