Facebook

Sunday 29 March 2015

Hii ndiyo simu iliyotengenezwa kwa kutumia nyasi.

Watu wengi wamekuwa wakilalamikia teknolojia na ufundi wa simu
nyingi za kisasa wengi wakiwaponda wabunifu kwa misingi ya kuwa
asilimia kubwa ya simu za mfumo wa 3G na zaidi zinatengezwa kwa
plastiki.

Sasa basi,bwana mmoja mbunifu amekuja na jibu ya kutengeza simu
kutokana na ''Nyasi'' .

Bwana Sean Miles amezindua simu itakayokuwa ya kipekee.
Simu hiyo ndiyo ya kwanza kuwahi kutengenezwa kwa asilimia 100%
kutokana na bidhaa hai.

Gamba la juu la simu hiyo limeundwa kwa bidhaa inayotokana na
nyasi maalum iliyochanganywa na kemikali fulani na kiungo (resin)
"mchanganyiko huu maalum unatoa sura kama vile (carbon) alisema
Miles.

Mfumo huo unachanganywa na kumbwa kwa njia itakayoruhusu
watengezaji wa simu kuumba gamba la simu inayotokana na nyasi.

Simu nyingi za kisasa hazina ubunifu na zinaelekea kufanana
Bwana Miles alikuwa amepewa kandarasi na kampuni ya simu ya O2
kutafuta mbinu ya kutumia upya bidhaa ambazo zimekosa wateja
ama zimezeeka.
Hata hivyo kitengo cha ubunifu kilitamaushwa na ubunifu wake na
sasa kimeanza mikakati ya kutathmini uwezo wa kampuni hiyo kuunda
kwa wingi magamba ya simu.

Kufikia sasa asilimia 25% ya simu nzee nchini uingereza
zinarekebishwa na kutumiwa upya.

0 comments:

Post a Comment