Facebook

Sunday 22 March 2015

CLASH OF THE TITANS: UCHAMBUZI WA MECHI YA EL CLASSICO NA Mr.CHOI (KAA TAARIFA YAKO)

   EL-CLASSICO ²  23:00
  BLAUGRANA vs BLANCOS
   Wakiwa katika dimba la Camp Nou lenye kuchukuwa watazamaji 99,354 huku wakishinda michezo 89 na kutoa sare 48 wakipoteza mara 92 Barcelona watawakabili Real na kujaribu kutafuta ushindi wa 90 ktk El Classico.
   Blaugrana wana pointi 65 huku Blancos wakishika nafasi ya pili kwa pointi 64 katika michezo mitano ya hivi karibuni kwenye mashindano mbalimbali Blancos wamekuwa wababe mbele ya Blaugrana kwani wameshinda mara tatu kati ya mbili walizo shinda Blaugrana na mchezo wa awamu ya kwanza Blancos walishinda 3-1.

  Ni miongoni mwa mchezo wenye kuteka hisia kubwa za mashabiki wa soka ulimwenguni kote si upinzani wa timu hizi tu bali hata upinzani wa safu za ushambuliaji kwa pande zote MSN-INTERNATIONAL ya Blaugrana na BBC ya Blancos pia sio safu hizo tu bali upinzani mwingine wa MESSI na C.Ronaldo.

   Messi ni kinara wa magoli La-Liga akiwa na magoli 32 dhidi ya 31 ya mpinzani wake Ronaldo hivyo licha ya upinzani wa timu hizi katka pointi tutaraji kuona wachezaji hawa kila mmoja akionesha umwamba mbele ya mwenzake.
  Cr7 ameshafunga magoli 6 ktk michezo 7 ndani ya Camp Nou huku akifunga mara 8 katika michuano yote na historia inaonesha amesha funga magoli 14 tangu atue Real na kucheza El Classico, tangu achukue tuzo ya mchezaji bora wa Dunia mwaka jana kiwango chake kimeonekana kushuka hasa kwa upande wa kuzifumania nyavu tofauti na mpinzani na hii leo endapo atafunga atafikisha goli la 15 sawa na Raul kwenye El Classico.

   Real wakiwa hawana matokeo mazuri kwa siku za hivi karibuni ndo timu pekee ilio ifunga Barca magoli mengi msimu huu (3-1) lakini pia watashuka dimbani kuitafuta historia ya mwaka 1978 kuifunga Barca mara tatu mfululizo kwenye El Classico kwani mwezi 10/2014 waliwafunga 3-1 na mwezi wa 4/2014 waliwafunga 2-1 ktk kombe la mfalme.

   Mara nyingi Real ama Blancos wamekuwa na asilimia 38 ya matokeo mazuri mbele ya Barca kipindi cha kwanza cha mchezo huku wapinzani wao asilimia 53 ya kipindi cha pili na zilizo baki ni sare. Majeruhi ni James lakini asilimia kubwa ya kikosi kipo fiti na tunataraji kuona Modriç na Kross wakicheza kati huku vita vikubwa vikiwa kwa Pepe na Suarez, Marcelo na Messi ingawa hofu ya Real ni golikipa Cassilas kwani amekuwa akifanya makosa sana golini.

     Blaugrana ama Barcelona wana Catalan wanaingia ktk mchezo huu wakiwa katika kiwango bora kwa sasa kikichagizwa na Messi alie funga magoli 17 kwenye michezo 11 La-liga tangu mwaka uanze,hawana majeraha ktk kikosi chao hasa kilicho cheza siku za hivi karibuni huku Busquets akirejea ingawa anaweza asipangwe leo na nafasi yake kucheza Mascherano.

  Mara nyingi Barca wakikutana na Real hasa siku za hivi karibuni safu yao ya ulinzi ndo imekuwa tatizo kwa kushindwa kuendana na kasi ya Cr7 na Bale ambao kwa staili ya mashambulizi ya kushtukiza na ya kasi wamekuwa na madhara sana.

  Pique ambae mara nyingi amekuwa akisababisha madhara kwa kushindwa kasi ya mchezo kwa hivi sasa yupo katika kiwango kizuri na uzuri huo atahitajika kudhirisha mbele ya BBC huku akitaraji simama na Mathieu.

   Wameruhusu magoli 16 mpaka sasa huku wakifunga magoli 78 pengine rekodi hiyo nzuri itawawezesha kuiboresha zaidi mbele ya Real.
    Magoli mengi ya Barca wamefunga hasa ndani ya kumi na nane tofauti na  Madrid ambao wanaonekana kufunga hasa nje ya kumi na nane. Mara ya mwisho Barca kupoteza michezo mingi ktk dimba la nyumbani ni msimu wa 2007/8 kipindi yupo Rijkaard baada ya kupoteza mara 3 kwenye ligi.

   Kiujumla mchezo utakuwa wa kasi sana kutokana na ushindani kwenye msimamo wa ligi Ratic, Iniesta katika safu ya kiungo cha juu na Modriç,Isco wote hawa wanatarajiwa kuonesha ufundi wa hali ya juu achilia mbali safu zao za MSN na BBC ambapo mpaka sasa MSN wanagoli 56 katika ligi na BBC wanagoli 55 zote ktk ligi pekee.

For more/ Ushauri::
Choikangta.ckt@gmail.com

0 comments:

Post a Comment