Facebook

Tuesday 31 March 2015

Azam FC- Hatujamzuia Kavumbagu Kwenda Burundi

Uongozi wa Azam FC umesema haujamzuia mshambuliaji wake wa kimataifa, Didier Kavumbagu kurejea kwao kuitumikia timu yake ya taifa ‘Entamba Murugamba’.Katika taarifa yake, Msemaji wa Azam FC Jaffar Idd Maganga,amesema Kavumbagu yuko Tanzania kwa
sababu ya uzembe wa Shirikisho la Soka Burundi.

Maganga amesema, amesema shirikisho hilo liliwasiliana na uongozi wa Azam FC likimuomba Kavumbagu kwa ajili ya kuitumikia timu yake ya taifa katika mechi ya kirafiki ya kalenda ya FIFA mwishoni mwa wiki hili tangu wakiwa Khartoum, Sudan wakicheza dhidi ya El-Merrikh,lakini mkali huyo wa mabao amekwama kwenda kutokana na kutotumiwa tiketi ya ndege.

0 comments:

Post a Comment