Facebook

Saturday, 14 March 2015

Chamberlain nje wiki nne.

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger atalazimika kujikuna kichwa baada
ya kupata habari kuwa kiungo chake cha kutegemewa Alex Oxlade-
Chamberlainhatakuwepo kwa takriban majuma tatu hadi nne zijazo
kutokana na jeraha nyuma ya goti.

Kulingana na kocha huyo,Chamberlain alipata jeraha hilo katika
mechi ya kukata na shoka ya FA dhidi ya wapinzani wao wa jadi
Manchester United jumatatu iliyopita.

Kujeruhiwa kwake ni pigo kwa azimio la Arsenal kuimarisha matokeo
yao katika ligi kuu ya Uingereza ambapo sasa wanashikilia nafasi ya
tatu .

Alex Oxlade-Chamberlain alichangia pakubwa katika ushindi wa 2-1
dhidi ya Manchester united katika FA
Aidha Arsenal wanajiandaa kwa mechi ya marudio ya mkondo wa 16
bora katika ligi kuu ya mabingwa barani Ulaya ambapo wameratibiwa
kuchuana dhidi ya Monaco juma lijalo.

Winga huyo alikuwa amerejea mwishoni mwa mwezi Februari baada ya
kukaa mwezi mmoja nje kufuata jeraha lengine la kiuno.
Wenger hata hivyo alipata afueni katika safu ya ulinzi baada ya
kurejea kwa Gabriel aliyejeruhiwa katika mechi ngumu dhidi ya QPR
mnamo Machi tarehe 4.

Related Posts:

  • Uholanzi yasonga mbele, Brazil Uholanzi ni timu ya kwanza kufuzu kwa mkondo wa pili wa kombe la dunia. Uholanzi ilitoka mabao 2-1, nyuma na kuishinda Australia mabao 3-… Read More
  • Siagi ya Uruguay yanaswa Brazil Siagi ya Uruguay ilinaswa na maafisa wa uwanja wa ndege Brazil Wasimamizi wa uwanja wa ndege Brazil wamezuia takriban kilo 39 za siagi ya… Read More
  • Okocha amlaumu kocha wa Nigeria. Nahodha wa zamani wa Nigeria Jay Jay Okocha amemlaumu kocha Stephen Keshi kwa timu yake kushindwa kucheza vizuri katika mechi yao ya kwanza ya Kombe la Dunia kundi F dhidi ya Iran siku ya Jumatatu. Timu hizo zilitok… Read More
  • Uingereza 1- 2 Uruguay Suarez ashangilia bao lake dhidi ya Uingereza Uruguay wameilaza Uingereza 2-1 katika mechi yao ya pili ya kundi D. Luiz Suarez ndiye amefunga mabao yote mawili ya Uruguay Uingereza walikuw… Read More
  • FIFA kuchunguza Mexico kwa ubaguzi Shirikisho la kandanda Duniani FIFA limeanza kuchunguza hatua ya kuiadhibu Mexico, baada ya madai kujitokeza kuwa mashabiki wake walihusika katika ma… Read More

0 comments:

Post a Comment