Facebook

Tuesday 31 March 2015

Hili ndilo Tamko la Maaskofu kuhusu sakata la Gwajima

Maaskofu kutoka madhehebu mbali mbali ya Kikristo nchini Tanzania wanakusudia kuonana na mkuu wa jeshi la polisi IGP Ernest Mangu,
ili kupata suluhu kuhusu sakata linalomkabili mkuu wa kanisa la ufufuo na uzima, askofu Josephat Gwajima.

Aidha, maaskofu hao pia wameonyesha masikitiko ya kile walichodai
kuwa ni vituo vya polisi kutoonekana kuwa ni mahali salama kwa
watuhumiwa wa makosa mbali mbali wanaofikishwa hapo.

Askofu Gwajima amelazwa katima hospitali ya TMJ jijini Dar es
Salaam, alikopelekwa kwa matibabu baada ya kuanguka na kupoteza
fahamu wakati akihojiwa na polisi, kwa tuhuma za kumkashifu askofu
wa kanisa katoliki jimbo kuu la Dar es Salaam, Muadhama Kadinali
Polycarp Pengo.

0 comments:

Post a Comment