Facebook

Monday 30 March 2015

Wanyama na Mitrovic mbioni kujiunga Arsenal.

Kiungo wa kati wa Southampton Mugubi Wanyama
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger anapanga kumnunua kiungo wa kati
wa Southampton Mkenya Victor Wanyama na mshambuliaji wa
Anderlecht Aleksandr Mitrovic kulingana na gazeti la the Sun nchini
Uingereza.

Wenger amejiandaa kutoa kitita cha pauni millioni 30 kwa wachezaji
hao wawili,huku Wanyama akigharimu kitita cha pauni millioni 20 naye
mshambuliaji huyo wa Anderlecht Mitrovic akigharimu pauni millioni
10.

Inaaminika kuwa Wanyama ataondoka katika kilabu ya Southampton iwapo atachukuliwa na klabu kikubwa huku naye Mitrovic akiwa
amekuwa akifuatiliwa na waajiri wa Arsenal katika kipindi cha wiki chache zilizopotea.
Mitrovic amekuwa akifananishwa na Didier Drogba kutokana na
mchezo wake.

0 comments:

Post a Comment