Facebook

Monday 30 March 2015

Dereva wa bodaboda anusurika kuuawa baada ya kupora mkoba.

kijana mmoja wa bodaboda maeneo ya Sinza
Afrikasana jijini DSM ambaye jina halikupatikana, alikoswakoswa
kuuawa baada ya kupora mkoba uliokuwa na simu ya mwanamke
aliyekuwa akipita njia.

Cha ajabu kijana huyo alivyokwapua mkoba,
pikipiki iligoma kuwaka basi raia wenye hasira kali wakaanza
kumshushia kipigo kikali.

Kijana aliponea chupuchupu kuchomwa moto,
kwani waliokuwa wamefuata mafuta ya petroli waliporudi walimkuta
trafiki akizuia asiuawe basi raia hao walihamishia hasira zao kwenye
kuichoma moto bodaboda ya kijana huyo.

0 comments:

Post a Comment