Facebook

Thursday 26 March 2015

FRANCE v BRAZIL , STADE DE FRANCE LEO USIKU, KUKUMBUSHIA FAINALI YA 1998(WORLD CUP)

Siku ya Alhamisi Usiku katika dimba la  Stade de France Jijini
Paris, ambako France Mwaka 1998
iliichapa Brazil 3-0 na kutwaa Kombe la
Dunia kwa mara ya kwanza na ya mwisho ,
ndio utakuwa Uwanja wa Mechi ya Kirafiki
kati ya miamba hao France na Brazil
ambao ni Mabingwa wa Dunia mara 5.

Ingawa Mechi hii ni ya Kirafiki lakini ni
muhimi kwa matayarisho ya Nchi hizi
kwani France ndio Wenyeji wa EURO 2016
Mwakani ambazo ndizo Fainali za Kombe
la Mataifa ya Nchi za Ulaya na Brazil
Mwezi Juni wako huko Chile kucheza Copa
America ambalo ndio Kombe la Mataifa ya
Nchi za Marekani ya Kusini .

Mara ya mwisho kwa Nchi hizi kukutana ni
Mwaka 2013 na Mabao ya Oscar , Hernanes
na Lucas Moura yaliwapa Brazil ushindi wa
3-0.

France , chini ya Kocha Didier Deschamps ,
watatinga kwenye Mechi hii bila ya
Wachezaji wao muhimu Kiungo Paul Pogba
na Kipa Hugo Lloris ambao ni Majeruhi
lakini wapo Mastaa wengine Kikosini kina
Patrice Evra, Antoine Griezmann na Karim
Benzèma.

Brazil, chini ya Kocha Dunga , wataongozwa
na Kapteni Neymar na Kikosini kwa mara
ya kwanza yupo Sentahafu wa Arsenal
Gabriel Paulista .

0 comments:

Post a Comment